വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സൂറത്തുൽ ഫജ്ർ   ആയത്ത്:

Surat Al-Fajr

وَٱلۡفَجۡرِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
kwa usiku upitapo na giza lake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali kupita kiasi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ukaletwa, Siku Hiyo kubwa, moto wa Jahanamu. Hiyo ndiyo Siku kafiri atakumbuka na kutubia. Kutamfalia nini sasa kukumbuka kwake na kutubia, na yeye katika ulimwengu alikuwa ameyapuuza hayo, na wakati wake umekwisha kupita?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atakuwa akisema: ‘Laiti mimi nilitanguliza ulimwenguni amali zenye kunifaa katika maisha yangu ya Akhera’.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Katika Siku Hiyo ngumu yenye vituko, hakuna atakaye kuweza kuadhibu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemuasi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Na hakuna atakaye kuweza kufunga kama kifungo Chake wala kufikia hadi yake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyotulia kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini Yeye na kuamini starehe ya Pepo Aliyowaandalia waumini!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rudi kwa Mola wako hali ya kuridhika na takrima ya Mwenyezi Mungu kwako na hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Ameridhika na wewe.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Ingia miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu walio wema
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
na ingia kwenye Pepo yangu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സൂറത്തുൽ ഫജ്ർ
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ ആശയ വിവർത്തനം സവാഹിലി ഭാഷയിൽ, ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്ർ, ശൈഖ് നാസിർ ഖമീസ് എന്നിവർ നിർവഹിച്ചത്

അടക്കുക