د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: الضحى   آیت:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
عربي تفسیرونه:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
عربي تفسیرونه:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
عربي تفسیرونه:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
عربي تفسیرونه:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
عربي تفسیرونه:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
عربي تفسیرونه:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
عربي تفسیرونه:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
عربي تفسیرونه:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimtende ubaya.
عربي تفسیرونه:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
عربي تفسیرونه:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: الضحى
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس - د ژباړو فهرست (لړلیک)

په سواهیلي ژبه کې د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، د ډاکټر عبدالله محمد ابوبکر او شیخ ناصر خمیس لخوا ژباړل شوی.

بندول