Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Balad   Versículo:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu.
Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na cheo chake.
Os Tafssir em língua árabe:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.
Os Tafssir em língua árabe:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.
Os Tafssir em língua árabe:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana awezae kumdhalilisha?
Os Tafssir em língua árabe:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.
Os Tafssir em língua árabe:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui yeyote hata huyo aliye muumba?
Os Tafssir em língua árabe:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya kutazamia,?
Os Tafssir em língua árabe:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
Na ulimi, na midomo miwili?
Na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?
Os Tafssir em língua árabe:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
Na tukambainishia zote njia mbili?
Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi yake.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya milimani?
Os Tafssir em língua árabe:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,
Os Tafssir em língua árabe:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kumlisha siku ya njaa
Au kumlisha siku ya njaa
Os Tafssir em língua árabe:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa,
Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.
Os Tafssir em língua árabe:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
Au masikini aliye vumbini.
Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.
Os Tafssir em língua árabe:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa mkono wa kulia.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa kheri na watapata adhabu.
Os Tafssir em língua árabe:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Balad
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar