Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Aladiyat (Ifarasi ziruka)   Umurongo:

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Na yeye ana pupa sana la mali.
Ibisobanuro by'icyarabu:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Aladiyat (Ifarasi ziruka)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga