Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Alhaaqat (Ukuri)   Umurongo:

Surat Al-Haqqah

ٱلۡحَآقَّةُ
Kiyama chenye kutukia kikweli ambacho ndani yake inahakikika ahadi ya Mwenyezi Mungu na onyo Lake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Kiyama chenye kutukia kikweli ni zipi sifa zake na hali zake?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Na kitu gani kilichokujulisha wewe, ewe Mtume, na kukueleza uhakika wa Kiyama na kikakupa wewe picha ya janga lake na shida zake?
Ibisobanuro by'icyarabu:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ
Thamūd, nao ni watu wa Ṣāliḥ, na ‘Ād, nao ni watu wa Hūd, walikikanusha Kiyama ambacho kinagonga nyoyo kwa vituko janga lake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ
Ama hao Thamūd waliangamizwa kwa ukelele mkubwa uliopita kiasi ukali wake,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ
na ama‘Ād waliangamizwa kwa upepo baridi unaovuma kwa nguvu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ
Mwenyezi Mungu Aliwasaliti nao masiku saba na michana minane yenye kufuatana, isiyokatika wala kusimama. Utawaona watu katika masiku hayo na michana wamekufa, kama kwamba wao ni vigogo mitende iliyo mibovu iliyolika ndani.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ
Basi je utamuona mtu yoyote miongoni mwao mwenye kusalia bila kuangamia?
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ
Na akaja mpita kiasi katika uasi Fir’awn na ummah waliomtangulia waliokanusha Mitume wao, na watu wakazi wa vijiji vya watu wa Lūṭ ambao majumba yao yaliwapindukia kwa sababu ya kitendo kibaya walichokifanya, cha ukafiri, ushirikina na mambo machafu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً
Kila ummah kati yao walimuasi mjumbe wa Mola wao ambaye alitumwa kwao, basi Mwenyezi Mungu Akawashika mshiko mkali mno.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ
Sisi, maji yalipopita kipimo chake, mpaka yakawa juu na kuangatika juu ya kila kitu, tuliwabeba watu wa asili zenu pamoja na Nūḥ ndani ya jahazi ambayo ilikuwa ndio sababu ya kuokoka Waumini na kuzamishwa makafiri,
Ibisobanuro by'icyarabu:
لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ
hili likiwa ni mazingatio na mawaidha, na lipate kulihifadhi tukio hilo kila shikio ambalo kazi yake ni kuhifadhi, na lielewe kile ambacho limekisikia.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ
Pindi Malaika atakapopuliza kwenye barugumu mpulizo mmoja, nao ni mpulizo wa kwanza ambao hapo patapatikana maangamivu ya ulimwengu,.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ
Na pindi ardhi na milima itakapoinuliwa kutoka mahali ilipo ikavunjwavunjwa na kugongwagongwa mara moja,
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Wakati huo Kiyama kitasimama.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ
Na mbingu zitafanya ufa na ziwe dhaifu na kulegea Siku hiyo, hazitakuwa na mshikamano wala ugumu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ
Na Malaika watakuwa kwenye pambizo na pande zake, na wataibeba «Arshi ya Mola wako juu yao Siku ya Kiyama Malaika wanane miongoni mwa Malaika wakubwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ
Katika Siku hiyo, mtaorodheshwa kwa Mwenyezi Mungu, enyi wat, ili mhesabiwe na mlipwe, hakuna chochote kitakachofichamana kwa Mwenyewzi Mungu miongoni mwa siri zenu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ
Ama yule Atakayepewa kitabu cha matendo yake kwa mkono wake wa kulia, atasema akiwa katika hali ya ubashasha na furaha, ‘Chukueni kitabu changu mkisome!
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ
Mimi nilikuwa na yakini duniani kuwa nitapata malipo yangu Siku ya Kiyama, nikajiandalia nayo kwa matayarisho ya Imani na matendo mema.»
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Basi yeye atakuwa kwenye maisha ya furaha ya kumridhisha;
Ibisobanuro by'icyarabu:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
kwenye Pepo ya juu kimahali na daraja;
Ibisobanuro by'icyarabu:
قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ
matunda yake yako karibu, anayachuma anayesimama, anayeketi na anayelala.
Ibisobanuro by'icyarabu:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ
Wataambiwa, «Kuleni na mnyweni kila aina ya vyakula na vinywaji, mkiwa mbali na kila kero, mkiwa mmesalimika na kila mnalolichukia, kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza siku za ulimwenguni.»
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ
Na ama yule atakayepewa kitabu cha matendo yake kwa mkono wake wa kushoto,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ
atasema akiwa katika hali ya kujuta na kupata hasara,
Ibisobanuro by'icyarabu:
يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ
«Natamani lau mimi sikupewa kitabu changu na sikujua malipo yangu! Natamani lau kile kifo nilichokufa duniani kilikuwa ndicho chenye kukata kabisa mambo yangu na nisifufuliwe baada yake!
Ibisobanuro by'icyarabu:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ
Mali yangu niliyoyakusanya hayakuninufaisha duniani!
Ibisobanuro by'icyarabu:
هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ
Hoja zangu zote zimenionokea, na sina hoja tena ya kuitumia kama hoja.»
Ibisobanuro by'icyarabu:
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
Hapo waambiwe walinzi wa Moto wa Jahanamu, «Mchukueni mhalifu huyu mfanya dhambi, ikusanyeni mikono yake shingoni mwake muitie pingu,
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ
kisha mtieni kwenye Moto unaowaka sana, apate kulihisi joto lake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ
Kisha mfungeni mnyororo wa chuma ambao urefu wake ni dhiraa sabini mumkokote nao na mumtie humo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ
Kwani yeye hakuwa akiamini kuwa Mwenyezi Mungu Ndiye Mola wa Haki, Peke Yake, Asiye na mshirika.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hakuwa akitenda matendo yanayoambatana na uongofu Wake, wala hakuwa akiwahimiza watu duniani kuwalisha wenye uhitaji miongoni mwa masikini na wengineo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ
basi kafiri huyu Siku ya Kiyama hatakuwa na jamaa wa karibu wa kumuepushia adhabu,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ
wala hatakuwa na chakula isipokuwa kile kinachotokana na usaa wa watu wa motoni,
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ
hakuna mwenye kukila isipokuwa wale wenye dhambi, wanaoshikilia kumkanusha Mwenyezi mungu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ
Naapa kwa mnavyoviona miongoni mwa vitu vinavyooonekana,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
na vile msivyoviona miongoni mwa vile vilivyoghibu kwenu., hakika Qur’ani ni maneno ya Mwenyezi Mungu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Inasomwa na mjumbe mkubwa wa cheo na utukufu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Na si maneno ya mshairi kama mnavyodai, ni uchache mno mnavyoamini.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si tungo kama zile tungo za makuhani, ni kuchache mno kule kukumbuka kwenu na kutia akilini kuwa kuna tafauti baina ya mawili hayo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Lakini hiyo Qur’ani ni maneno ya Mola wa viumbe wote Aliyoyateremshia Mtume Wake Muhaammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na lau Muhammad angalitusingizia maneno tusiyoyanena
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
tungalimtesa na tungalimkamata kwa nguvu na uweza, kwani nguvu ya kila kitu iko kwenye upande wake wa kulia,
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
kisha tungalimkata mshipa wa moyo wake.,
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
hataweza yoyote kuyazuia mateso yetu yasimpate.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na hii Qur’ani ni mawaidha kwa wachamungu wanaofuata amri za Mwenyezi Mungu na kuyaepuka makatazo yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na sisi kwa hakika tunajua kwamba miongoni mwenu kuna wanaoikanusha hii Qur’ani pamoja na kuwa dalili zake ziko wazi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na kwa hakika kuikanusha Qur’ani ni majuto makubwa kwa wenye kuikanusha pindi watakapoiona adhabu yao na kuona starehe za wenye kuiamini.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na kwa hakika hii Qur’ani ni haki iliyothibiti na yakini isiyo na shaka.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi Mwepushie Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kila sifa isiyonasibiana na haiba Yake, na umtaje kwa jina Lake tukufu.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Alhaaqat (Ukuri)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga