Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis * - Ishakiro ry'ibisobanuro


Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al Qiyamat (Izuka)   Umurongo:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Siku ya Hesabu na Malipo,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
na Anaapa kwa nafsi yenye kuamini na kuchamungu, inayomlaumu mwenyewe kwa kuacha matendo ya utiifu na kufanya matendo yenye kuangamiza, kwamba watu watafufuliwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Je anadhanihuyu binadamu kafiri kuwa sisi hatutaweza kuikusanya mifupa yake baada ya kuwa mbalimbali.?
Ibisobanuro by'icyarabu:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Ndio! Tutaikusanya na tunaweza kufanya vidole vyake au ncha za vidole vyake- baada ya kuvikusanya na kuzioanisha- viwe kwenye umbo la sawasawa, kama vilivyokuwa kabla ya kufa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Bali binadamu anakanusha kufufuliwa, anataka asalie kwenye kufanya ubaya kwa siku za mbeleni za maisha yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Kafiri huyu huwa akiuliza, akiliona jambo la kusimama Kiyama kuwa liko mbali, «Ni lini Siku ya Kiyama?’
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi macho yatakapoduwaa na yakashituka kwa kutishika na kile yalichokiona cha vituko vya Siku ya Kiyama,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
na ukafutika mwangaza wa mwezi,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
na vikakusanywa jua na mwezi katika kukosa mwangaza, kikawa kila mojawapo ya hivyo viwili hakina mwangaza,
Ibisobanuro by'icyarabu:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
wakati huo binadamu atasema, «Pa kukimbilia ni wapi kuiepuka adhabu?»
Ibisobanuro by'icyarabu:
كَلَّا لَا وَزَرَ
Mambo sivyo kama unavyotamani yawe, ewe binadamu, ya kutaka kukimbia. Huna mahali pa kukimbilia wala pa kupata uokozinfsi yake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake ndio mwisho wa viumbe Siku ya Kiyama na ndipo mahali pao pa kutulia, na hapo Amlipe kila mtu kwa kile alichostahiki.
Ibisobanuro by'icyarabu:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Atapashwa habari binadamu Siku hiyo kwa matendo yake yote, mema na mabaya, aliyoyatanguliza miongoni mwa hayo katika maisha yake na aliyoyachelewesha.
Ibisobanuro by'icyarabu:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali binadamu ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake, yenye kumfuata kwa alichokitenda na alichokiacha,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
hata kama atakuja na kila udhuru wa kuelezea sababu ya uhalifu wake, hilo halitamfaa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usitikise, ewe Nabii, ulimi wako kwa Qur’ani wakati wahyi unapoteremka ili ufanye haraka kuihifadhi kwa kuogopa isikuponyoke.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Kwani ni juu yetu sisi kuikusanya kwenye kifua chako kisha uisome kwa ulimi wako wakati utakapo. Mjumbe wetu Jibrili akikusomea,
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
basi kisikilize kisomo chake na umpulikize. Kisha isome kama alivyokusomea,
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
kisha ni juu yetu kukuelezea kilichokutatiza kukifahamu katika maana yake na hukumu zake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Mambo sivyo kama mlivyodai, enyi mkusanyiko wa washirikina, kuwa hakuna kufufuliwa wala kulipwa.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Bali nyinyi ni watu mnaopenda dunia na pambo lake na mnaacha Akhera na starehe zake.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Nyuso za watu wema Siku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kung’ara, nzuri na zenye furaha,
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
zitamuona Mola Aliyeziumba na Anayezimiliki, na zitastarehe kwa hilo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Nyuso za watu wabaya Silku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kukunjana na kusinyaa,
Ibisobanuro by'icyarabu:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
zinatazamia kushukiwa na msiba mkubwa wenye kuvunja.
Ibisobanuro by'icyarabu:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
Ni kweli! Pindi roho itakapofika sehemu za juu za kifua,
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
na wakasema baadhi ya waliohudhuria kuwaambia wengine, «Je kuna mtu wa kumzungua na kumpoza kutokana na hali hii aliyonayo?»
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na yule ambaye yuko katika hali ya kufa akajua kwamba lile lililomshukia ni kuaga dunia, kwa kuwa anawaona Malaika wa mauti.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na ikashikana shida ya mwisho wa duniani na shida ya mwanzo wa Akhera. Kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
Ibisobanuro by'icyarabu:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Watu watapelekwa Siku ya Kiyama: ima Peponi au Motoni.
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Hakuwa kafiri ni mwenye kumuamini Mtume na Qur’ani, wala hakuwa ni mwenye kumtekelezea Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Swala za faradhi.
Ibisobanuro by'icyarabu:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Lakini aliikanusha Qur’ani na akaipa mgongo Imani,
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
kisha akaenda kwa watu wake akijiona hali ya kujigamba katika kutembea kwake. Basi maangamivu
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
ni yako baada ya maangamivu!
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha maangamivu ni yako baada ya maangamivu!
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Je anadhani huyu binadamu anayekanusha kufufuliwa kuwa ataachwa bure: haamrishwi wala hakatazwi, hahesabiwi wala hateswi?
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa binadamu huyu ni tone la manii dhaifu linalotokana na maji matwevu yanayomwagwa na kumiminwa kwenye kizazi,
Ibisobanuro by'icyarabu:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
kisha yakawa ni kipande cha damu iliyo kavu. Mwenyezi Mungu Akaliumba kwa uweza Wake na Akazilinganisha sura zake katika umbo la mwili lililo zuri kabisa?
Ibisobanuro by'icyarabu:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Akafanya kutokana na binadamu huyu jinsi mbili: ya kiume na ya kike. Je kwani hakuwa Mola huyo Muumba wa vitu hivyo ni Muweza wa kuwarudisha viumbe wakiwa hai baada ya kutoweka kwao.
Ibisobanuro by'icyarabu:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Ndio! Anaweza. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hakika ni Muweza wa hilo.
Ibisobanuro by'icyarabu:
 
Ibisobanuro by'amagambo Isura: Al Qiyamat (Izuka)
Urutonde rw'amasura numero y'urupapuro
 
Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro mu giswahili - abdullah muhamad na nasoor khamis - Ishakiro ry'ibisobanuro

Guhindura ibisobanuro bya Quran mu giswahili byasobanuwe na Dr Abdallah Mohamed abubakar na nassor khamis

Gufunga