Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Përmbajtja e përkthimeve

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu El Lejl   Ajeti:

Surat Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika!
Naapa kwa usiku kinapo enea kiza chake!
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri!
Na naapa kwa mchana unapo zagaa mwangaza wake!
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
Na naapa kwa Mjuzi aliye umba viwili viwili, dume na jike, katika kila vinavyo zaliwa!
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
Hakika juhudi zenu bila ya shaka zimekhitalifiana; kwani wapo wenye kubahatika katika juhudi zao, na wako wasio bahatika.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu!
Ama mwenye kutoa katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na akamkhofu Mola wake Mlezi, na kwa hivyo akaepuka anayo yakataza,
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akaliwafiki lilio jema!
Na akayakinika kufuata fadhila njema, nayo ni Imani kumuamini Mwenyezi Mungu kwa kumjua,
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
Basi Sisi tutamtengenezea awe katika khulka ya wepesi na raha kwa kumwongoza kwenye njia ya kheri.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake!
Ama mwenye kufanya ubakhili kwa mali yake asitoe haki ya Mwenyezi Mungu iliomo humo, na akawa hana haja na yatokayo kwa Mwenyezi Mungu,
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akakanusha lilio jema!
Na akakadhibisha khulka nzuri,
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mazito!
Basi huyo tutamtengenezea khulka ambayo inapelekea uzito na mashaka ya milele.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
Na kitu gani katika adhabu ambacho hayo mali yake yataweza kumkinga nacho, atapo teketea yeye mwenyewe mzima?
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
Hakika ni juu yetu, Sisi, kwa kufuatana na hikima yetu, ndio tuwabainishie viumbe njia ya uwongofu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
Na juu yetu Sisi peke yetu, bila ya shaka, hili jambo la kuendesha yaliomo duniani na Akhera.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
Ndio maana tukakutieni khofu ya Moto unao waka na kuripuka!
Tefsiret në gjuhën arabe:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hatauingia ila mwovu kabisa!
Hawauingii kwa kudumu ila kafiri
Tefsiret në gjuhën arabe:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
Aliye ikadhibisha Haki na akazipuuza Ishara za Mola wake Mlezi.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na mchamngu ataepushwa nao,
Na atakuwa mbali na huo Moto aliye mwingi wa kujikinga na ukafiri na maasi,
Tefsiret në gjuhën arabe:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
Amabye hutoa mali yake wakati wa nafasi ili kujisafisha na uchafu wa ubakhili, na najsi ya uchoyo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
Na mtoaji huyu si kama anaye mtu yeyote ambaye ndio anamlipa kwa neema aliyo mfanyia zamani,
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
Bali anatoa hicho kwa kutafuta radhi ya Mola wake Mlezi Mtukufu tu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
Naye atakuja ridhika!
Na bila ya shaka atakuja pata kutoka kwa Mola wake Mlezi anacho kitaka kwa njia za ukamilifu kabisa, hata itimie radhi kwake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu El Lejl
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Përmbajtja e përkthimeve

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Mbyll