పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ * - అనువాదాల విషయసూచిక


భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: సూరహ్ అన్-నాజిఆత్   వచనం:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi Peponi ndiko makazi yake.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
అరబీ భాషలోని ఖుర్ఆన్ వ్యాఖ్యానాలు:
 
భావార్ధాల అనువాదం సూరహ్: సూరహ్ అన్-నాజిఆత్
సూరాల విషయసూచిక పేజీ నెంబరు
 
పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్ - అనువాదాల విషయసూచిక

ఖురాన్ అర్థాలను స్వాహిలీలోకి అనువదించడం,దాని అనువాదకులు డా: అబ్దుల్లా ముహమ్మద్ అబూబకర్ మరియు నాసిర్ ఖుమైస్

మూసివేయటం