Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: At-Takwīr   Ayah:

Surat At-Takwir

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
Ang mga Tafsir na Arabe:
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
Ang mga Tafsir na Arabe:
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: At-Takwīr
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara