Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Sure: Sûretu Abese   Ayet:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka!
Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,
Arapça tefsirler:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.
Arapça tefsirler:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,
Arapça tefsirler:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Au atawaidhika na mawaidha yamfae.
Arapça tefsirler:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja!
Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake,
Arapça tefsirler:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia?
Wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.
Arapça tefsirler:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?
Arapça tefsirler:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi .
Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu,
Arapça tefsirler:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa!
Naye anamkhofu Mwenyezi Mungu .
Arapça tefsirler:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza?
Wewe unampuuza.
Arapça tefsirler:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Hakika Aya hizi ni mawaidha.
Arapça tefsirler:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke.
Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.
Arapça tefsirler:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,
Arapça tefsirler:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.
Arapça tefsirler:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;
Arapça tefsirler:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema.
Walio bora, wema.
Arapça tefsirler:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?
Arapça tefsirler:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?
Arapça tefsirler:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.
Arapça tefsirler:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.
Arapça tefsirler:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!
Arapça tefsirler:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.
Arapça tefsirler:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.
Arapça tefsirler:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani,
Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.
Arapça tefsirler:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende,
Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,
Arapça tefsirler:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,
Arapça tefsirler:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama;
Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).
Arapça tefsirler:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.
Arapça tefsirler:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele,
Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,
Arapça tefsirler:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake,
Arapça tefsirler:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye,
Na mama yake, na baba yake,
Arapça tefsirler:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe.
Na mkewe, na wanawe!
Arapça tefsirler:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha
Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!
Arapça tefsirler:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza,
Arapça tefsirler:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka;
Zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.
Arapça tefsirler:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika,
Zimegubikwa na kiza na weusi.
Arapça tefsirler:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu
Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu Abese
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat