قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە ئەئلا   ئايەت:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa!
Litakase jina la Mola wako Mlezi lilio tukufu na kila kitu kisicho kuwa kinaelekeana nalo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliye umba, na akaweka sawa!
Aliye umba kila kitu, na akajaalia uumbaji wote sawa sawa katika hukumu na kupangana.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,.
Na akakadiria kwa kila kitu kwa mujibu wa maslaha yake, na akakiongoza.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na aliye otesha malisho!
Na ambaye akatoa kwenye ardhi mimea namna mbali mbali ya kuwalisha wanyama.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
Na akaifanya mimea hiyo baada ya kuwa kijani imestawi, ikakauka na imekuwa myeusi!
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomesha wala hutasahau!
Ewe Muhammad! Sisi tutakujaalia uwe ni mwenye kuisoma Qur'ani kwa ufunuo kutoka kwetu, na wala hutosahau utacho kihifadhi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
Isipo kuwa anacho taka Mwenyezi Mungu ukisahau, kwani hakika Yeye Mtukufu anayajua wanayo yadhihirisha waja wake na wanayo yaficha, ikiwa maneno au vitendo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
Na tutakuwezesha kupita njia ya kufikilia kwa wepesi mambo yako yote.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
Basi wakumbushe watu ikiwa kukumbusha kutaleta manufaa, kwani inavyo faa ndio kuwanafiisha.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
Watanafiika kwa ukumbusho wako wanao mwogopa Mwenyezi Mungu.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
Na atajitenga na ukumbusho mpotovu anaye shikilia kufanya inda na ukafiri.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
Ambaye ataingia kwenye Moto mkubwa ulio andaliwa kuwa ndio malipo yake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
Tena hatokufa huko Motoni akapumzika kwa kifo, wala hawi hai kwa uhai wa kustarehe nao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
Hakika amefuzu mwenye kujisafisha na ukafiri na maasi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akaswali.
Na akalikumbuka jina la Muumba wake kwa moyo wake na ulimi wake, na akaswali kwa unyenyekevu kama itakikanavyo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
Bali nyinyi hamfanyi hayo yanayo pelekea kufanikiwa, lakini katika hima zenu mnatanguliza maisha ya duniani kuliko ya Akhera.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
Na Akhera ni bora kuliko dunia, kwa usafi wa neema zake, na ni yenye kubaki na kudumu zaidi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
Hakika haya yote yaliyo tajwa katika Sura hii bila ya shaka yamethibitishwa katika Vitabu vya zamani,
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Vitabu vya Ibrahimu na Musa; kwani haya yamewafikiana na mafunzo ya dini zote na yamesajiliwa katika Vitabu vya mbinguni.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە ئەئلا
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

تاقاش