قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ عادیات   آیت:

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
عربی تفاسیر:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
عربی تفاسیر:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
عربی تفاسیر:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
عربی تفاسیر:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
عربی تفاسیر:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
عربی تفاسیر:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
عربی تفاسیر:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Na yeye ana pupa sana la mali.
عربی تفاسیر:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
عربی تفاسیر:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
عربی تفاسیر:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ عادیات
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں