قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ قارعہ   آیت:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Kiyama chenye kugonga nyoyo za watu kwa vituko vyake.
عربی تفاسیر:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Ni kitu gani hiko chenye kugonga?
عربی تفاسیر:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na ni lipi lililokujulisha ni kipi hiko chenye kugonga?
عربی تفاسیر:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku hiyo watu watakuwa , kwa wingi wao, kugawanyika kwao na kuzunguka kwao, ni kama pandzi walioenea. Nao ni wale wanaojitupa motoni.
عربی تفاسیر:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na majabali yatakuwa ni kama pamba yenye rangi tofauti inayochambuliwa kwa mkono ikawa ni mapepe na ikamalizika.
عربی تفاسیر:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi mwenye kuwa mizani za mema yake ni nzito,
عربی تفاسیر:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
atakuwa kwenye maisha ya kuridhika Peponi.
عربی تفاسیر:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Ama mwenye kuwa mizani za mema yake ni nyepesi na mizani za maovu yake ni nzito,
عربی تفاسیر:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
makazi yake yatakuwa ni Moto wa Jahanamu.
عربی تفاسیر:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Ni lipi lililokujulisha, ewe Mtume, ni ipi hii Jahanamu inayoitwa «Hāwiyah»?
عربی تفاسیر:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto unaowaka sana kwa kuni ziliomo ndani yake.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ قارعہ
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں