قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ علَق   آیت:

Surat Al-Alaq

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba.
عربی تفاسیر:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu.
عربی تفاسیر:
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu.
عربی تفاسیر:
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu.
عربی تفاسیر:
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu.
عربی تفاسیر:
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
عربی تفاسیر:
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
akijiona ametosheka kwa utajiri wake.
عربی تفاسیر:
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda.
عربی تفاسیر:
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl,
عربی تفاسیر:
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake?
عربی تفاسیر:
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza?
عربی تفاسیر:
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo?
عربی تفاسیر:
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo,
عربی تفاسیر:
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya?
عربی تفاسیر:
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni.
عربی تفاسیر:
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa.
عربی تفاسیر:
فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye.
عربی تفاسیر:
سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu.
عربی تفاسیر:
كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ علَق
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں