قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ قارعہ   آیت:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Inayo gonga!
AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.
عربی تفاسیر:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!
عربی تفاسیر:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?
عربی تفاسیر:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!
عربی تفاسیر:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.
عربی تفاسیر:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,
عربی تفاسیر:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.
عربی تفاسیر:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,
عربی تفاسیر:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.
عربی تفاسیر:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?
عربی تفاسیر:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!
Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: سورۂ قارعہ
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں