Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний * - Таржималар мундарижаси

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Маънолар таржимаси Сура: Тур сураси   Оят:

Surat At-Tur

وَٱلطُّورِ
Naapa kwa mlima wa T'ur!
Ninaapa kwa mlima wa T'ur ulioko katika Sinai. Kwenye mlima huo ndio Nabii Musa a.s. alisemezwa.
Арабча тафсирлар:
وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ
Na Kitabu kilicho andikwa .
Ninaapa kwa mlima wa T'ur ulioko katika Sinai. Kwenye mlima huo ndio Nabii Musa a.s.
Арабча тафсирлар:
فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ
Katika ngozi iliyo kunjuliwa!
Kilicho andikwa katika kurasa zilio nyepesi kuzisoma,
Арабча тафсирлар:
وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ
Na kwa Nyumba iliyo jengwa!
Na kwa Nyumba iliyo jengwa kwa sababu ya wenye kuizunguka kwa ibada na wenye kusimama na kurukuu na kusujudu kwa Swala,
Арабча тафсирлар:
وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa!
Na naapa kwa mbingu iliyo nyanyuliwa bila ya nguzo, na bahari iliyo jaa.
Арабча тафсирлар:
وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ
Na kwa bahari iliyo jazwa!
Na bahari iliyo jaa.
Арабча тафсирлар:
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi waliyo ahidiwa makafiri bila ya shaka itawateremkia hapana hivi wala hivi.
Арабча тафсирлар:
مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ
Hapana wa kuizuia.
Hapana wa kuizuia isiwafikilie.
Арабча тафсирлар:
يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso!
Siku mbingu itapo tikisika kwa mtikiso mkubwa.
Арабча тафсирлар:
وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
Na milima itapo ng'oka kutoka hapo ilipo kwa kuonekana khasa.
Арабча тафсирлар:
فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
Maangamio makubwa yatawapata siku hiyo hao wanao kadhibisha Haki.
Арабча тафсирлар:
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
Ambao katika upotovu ndio mchezo wao wanapo chezea.
Арабча тафсирлар:
يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
Siku watakapo sukumwa kuingizwa Motoni kwa nguvu.
Арабча тафсирлар:
هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
Wataambiwa: Huu ndio Moto mlio kuwa mkiukanusha duniani.
Арабча тафсирлар:
أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
Je! Bado mnaendelea kuukanya. Huu Moto mnao uona ni uchawi, au hamwoni tu?
Арабча тафсирлар:
ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
Uingieni, mpate kuonja vukuto lake. Mkivumilia shida zake, au mkitovumilia, kwenu ni mamoja. Hakika leo mtayakuta mliyo kuwa mkiyatenda duniani.
Арабча тафсирлар:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَعِيمٖ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani yenye wasaa, hapana awezae kuyaeleza yalivyo, na neema kubwa kadhaalika.
Арабча тафсирлар:
فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
Wakistarehe na neema alizo wapa Mola wao Mlezi, na Mola wao Mlezi akawalinda na adhabu ya Moto.
Арабча тафсирлар:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
Wataambiwa: Kuleni chakula mpendacho, na kunyweni kwa raha, kuwa ni malipo ya vitendo mlivyo vitenda duniani.
Арабча тафсирлар:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
Wakikaa nao wameegema juu ya makochi yaliyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza wake weupe wenye macho ya vikombe wazuri.
Арабча тафсирлар:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
Na walio amini, na wakastahiki vyeo vya juu, na vizazi vyao wakawafuata katika Imani, na wao hawajafikia daraja zile za baba zao, tutawakutanisha nao hao dhuriya zao, wapate kutulia nyoyo zao. Na wala hatuwapunguzii chochote katika thawabu za vitendo vyao. Wala wazazi hawatobeba chembe katika makosa ya dhuriya zao. Kwa sababu kila mtu amefungamana kwa rahani na vitendo vyake visio bebwa na mwenginewe.
Арабча тафсирлар:
وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
Na tutawazidishia matunda mengi, na nyama kama waipendayo.
Арабча тафсирлар:
يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
Huko Peponi watakuwa wakipeana kwa mapenzi bilauri zilio jaa vinywaji visio leta maneno yasiyo na maana wala vitendo vya dhambi, yaani havilevi na kuondoa akili.
Арабча тафсирлар:
۞ وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
Na watakuwa wakiwapitia vijana walio wekwa kwa kuwatumikia, kwa weupe wao na usafi wao kama lulu iliomo ndani ya chaza.
Арабча тафсирлар:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wakiulizana.
Na watu wa Peponi watakabiliana wakiulizana wao kwa wao khabari za hayo mambo makuu wanayo yapata na sababu zake.
Арабча тафсирлар:
قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
Kabla ya neema hizi sisi tulikuwa pamoja na ahali zetu tukiiogopa adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Арабча тафсирлар:
فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
Mwenyezi Mungu akatufadhili kwa rehema yake, na akatukinga na adhabu ya Moto.
Арабча тафсирлар:
إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
Hakika sisi kabla ya haya tulikuwa duniani tukimuabudu Yeye tu. Yeye peke yake ndiye Mhisani Mkunjufu wa rehema.
Арабча тафсирлар:
فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
Wewe endelea na kukumbusha kama unavyo fanya. Kwani wewe, kwa neema ya Mwenyezi Mungu aliyo kuneemesha kukupa Unabii na akili iliyo timia, si kuhani anaye toa khabari za ghaibu bila ya ilimu, wala si mwendawazimu unaye sema usiyo yasadiki.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
Bali ati wanasema huyu ni mtunga mashairi, tunaye mngojea afikiwe na mauti!
Арабча тафсирлар:
قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
Waambie kwa kuwatisha: Ngojeeni, na mimi nami ni katika wanao ngojea mwisho wa hali yangu na hali yenu!
Арабча тафсирлар:
أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
Bali ndio akili zao zinawaamrisha waseme maneno hayo yanayo gongana. Kwani kohani na mtunga mashairi ni watu wenye fahamu na akili; na mwendawazimu hana akili. Lakini hawa ni watu walio pita mipaka katika inadi zao.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
Bali ati wanasema: Muhammad ameizua hii Qur'ani! Bali hawa kwa ukaidi wao hawaamini tu.
Арабча тафсирлар:
فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
Basi nawalete masimulizi kama haya ya Qur'ani, ikiwa wao ni wasema kweli kuwa Muhammad kaizua.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
Kwani wao wameumbwa bila ya kuweko Muumbaji, au wao wamejiumba wenyewe, basi kwa hivyo ati ndio hawamtambui Muumbaji wa kumuabudu?
Арабча тафсирлар:
أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
Kwani wao ndio walio ziumba mbingu na ardhi kwa uumbaji mzuri wa pekee wa namna hii? Bali wao hawana na yakini na lolote lilio mwajibikia Muumbaji. Na kwa hivyo ndio wanamshirikisha.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
Kwani wao wanazo khazina za Mola wako Mlezi wanazo zisarifu watakavyo? Au wana nguvu za kutenda watakavyo, na kupanga mambo kama wapendavyo?
Арабча тафсирлар:
أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
Bali wanacho kipandio cha kupandia mpaka mbinguni wakasikiliza anayo yahukumia Mwenyezi Mungu? Kama hivyo, basi nawamlete huyo mtu wao anaye sikiliza atoe hoja iliyo wazi kuthibitisha madai yake.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
Ati Mwenyezi Mungu ndiye mwenye mabinti, kama mnavyo zua, na nyinyi ndio mna watoto wa kiume kama ndio mnavyo penda?
Арабча тафсирлар:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
Kwani wewe unawaomba chochote kuwa ni ujira wa kuwafikishia Ujumbe wako, ndio wamethakilika na hizo gharama wakalalimika?
Арабча тафсирлар:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
Bali kwani wao wanao ujuzi kujua mambo ya ghaibu, yaliyo fichikana, na hivyo wanaandika kutoka hayo wayatakayo?
Арабча тафсирлар:
أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
Au wanataka kukufanyia vitimbi tu na kuuharibu Ujumbe wako? Basi hao walio kufuru ndio wanao stahiki kutumbukia katika vitimbi vyao.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
Au wao wanae mungu wa kuabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu atakae walinda na adhabu ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu ametakasika na hayo wanayo mshirikisha naye!
Арабча тафсирлар:
وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
Na wakiona kipande cha mbingu kinwaangukia kuwaadhibu wao husema, kwa inda tu: Ni mawingu yaliyo bebana!
Арабча тафсирлар:
فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
Waache bila ya kuwajali mpaka watakapo ikuta siku yao watapo angamizwa.
Арабча тафсирлар:
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
Siku ambayo hila zao hazitawakinga hata na chembe ya adhabu, wala hawatapata wa kuwanusuru.
Арабча тафсирлар:
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
Na hakika hao walio dhulumu watapata adhabu mbali na hii waliyo teseka nayo hapa duniani, lakini wengi wao hawajui hayo.
Арабча тафсирлар:
وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
Wewe isubirie hukumu ya Mola wako Mlezi ya kuwapa muhula hao, na wewe kupata maudhi yao. Kwani hakika wewe umo katika hifadhi yetu na ulinzi wetu. Basi vitimbi vyao havitokudhuru wewe. Na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo amka.
Арабча тафсирлар:
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
Na tafuta usiku usiku nafasi ya kumsabihi, yaani kumtakasa, Mwenyezi Mungu, na mtakase pia wakati zinapo kuchwa nyota, yaani alfajiri.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Тур сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржим: Али Муҳсин ал-Бервааний

Ёпиш