Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний * - Таржималар мундарижаси

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Маънолар таржимаси Сура: Муддассир сураси   Оят:

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliye jigubika!
Арабча тафсирлар:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Simama uonye!
Арабча тафсирлар:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
Арабча тафсирлар:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na nguo zako, zisafishe.
Арабча тафсирлар:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na yaliyo machafu yahame!
Арабча тафсирлар:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
Арабча тафсирлар:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
Арабча тафсирлар:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Basi litapo pulizwa barugumu,
Арабча тафсирлар:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
Арабча тафсирлар:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
Арабча тафсирлар:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache peke yangu na niliye muumba;
Арабча тафсирлар:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
Арабча тафсирлар:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
Na wana wanao onekana,
Арабча тафсирлар:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Kisha anatumai nimzidishie!
Арабча тафсирлар:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
Арабча тафсирлар:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
Арабча тафсирлар:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
Арабча тафсирлар:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha akatazama,
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
Арабча тафсирлар:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
Арабча тафсирлар:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
Арабча тафсирлар:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
Арабча тафсирлар:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
Арабча тафсирлар:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haubakishi wala hausazi.
Арабча тафсирлар:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
Арабча тафсирлар:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Juu yake wapo kumi na tisa.
Арабча тафсирлар:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
Арабча тафсирлар:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
Арабча тафсирлар:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
Na kwa usiku unapo kucha!
Арабча тафсирлар:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
Арабча тафсирлар:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
Арабча тафсирлар:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
Ni onyo kwa binaadamu,
Арабча тафсирлар:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
Арабча тафсирлар:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
Арабча тафсирлар:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
Арабча тафсирлар:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
Арабча тафсирлар:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Khabari za wakosefu:
Арабча тафсирлар:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
Арабча тафсирлар:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakiswali.
Арабча тафсирлар:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
Арабча тафсирлар:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
Арабча тафсирлар:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
Арабча тафсирлар:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
Арабча тафсирлар:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
Арабча тафсирлар:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
Арабча тафсирлар:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
Арабча тафсирлар:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
Wanao mkimbia simba!
Арабча тафсирлар:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
Арабча тафсирлар:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
Арабча тафсирлар:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
Арабча тафсирлар:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye taka atakumbuka.
Арабча тафсирлар:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Муддассир сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржим: Али Муҳсин ал-Бервааний

Ёпиш