Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (15) Chương: Chương Al-Fat-h
سَيَقُولُ ٱلۡمُخَلَّفُونَ إِذَا ٱنطَلَقۡتُمۡ إِلَىٰ مَغَانِمَ لِتَأۡخُذُوهَا ذَرُونَا نَتَّبِعۡكُمۡۖ يُرِيدُونَ أَن يُبَدِّلُواْ كَلَٰمَ ٱللَّهِۚ قُل لَّن تَتَّبِعُونَا كَذَٰلِكُمۡ قَالَ ٱللَّهُ مِن قَبۡلُۖ فَسَيَقُولُونَ بَلۡ تَحۡسُدُونَنَاۚ بَلۡ كَانُواْ لَا يَفۡقَهُونَ إِلَّا قَلِيلٗا
Watasema wale walioachwa nyuma utakapoondoka, ewe Nabii, wewe na Maswahaba wako kuelekea kwenye ngawira za Khaybar ambazo Mwenyezi Mungu Aliwaahidi nyinyi kuwa mtazipata, «Tuacheni tuende na nyinyi huko Khaybar» wakiwa wanataka kwa hilo kubadilisha ahadi ya Mwenyezi Mungu kwenu. Waambie, «Hamtatoka pamoja na sisi kwenda Khaybar, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Alitwambia kabla hatujarudi Madina kwamba ngawira za Khaybar ni za wale waliohudhuria Ḥudaybiyah pamoja na sisi.» Watasema, «Mambo sivyo kama mnavyosema. Mwenyezi Mungu Hakuwaamrisha nyinyi hili. Nyinyi mnatukataza kutoka na nyinyi kwa uhasidi wenu tusije tukapata ngawira pamoja na nyinyi.» Mambo sivyo kama walivyodai, bali wao walikuwa hawaelewi amri za Mwenyezi Mungu kuhusu haki zao na wajibu wao wa kidini isipokuwa kidogo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (15) Chương: Chương Al-Fat-h
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại