Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (5) Chương: Chương Al-Ma-idah
ٱلۡيَوۡمَ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُۖ وَطَعَامُ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حِلّٞ لَّكُمۡ وَطَعَامُكُمۡ حِلّٞ لَّهُمۡۖ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِيٓ أَخۡدَانٖۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ حَبِطَ عَمَلُهُۥ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ
Na miongoni mwa ukamilifu wa neema ya Mwenyezi Mungu kwenu leo hii, enyi Waumini, ni kwamba Amewahalalishia vilivyo halali vizuri. Na vichinjwa vya Mayahudi na Wanaswara, iwapo watawachinja wanyama wao kuambatana na sheria yao, ni halali kwenu ; na vichinjwa vyenu ni halali kwao. Na Amewahalalishia nyinyi, enyi Waumini, kuwaoa wanawake wanaojihifadhi, nao ni wale walio huru kati ya wanawake Waumini wanaojizuia na uzinifu. Vilevile ni halali kuwaoa wanawake walio huru wanaojiepusha na uzinifu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, iwapo mtawapa mahari yao na mkawa mumejihifadhi kwa kutofanya uzinifu na kuweka mahawara na mkawa mumejiaminisha kuwa hamutaathirika na dini yao. Na mwenye kuzikataa sheria za fmani, basi vitendo vyake vimishaharibika, na yeye, Siku ya Kiyama, atakuwa ni miongoni mwa wenye kupata hasara.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (5) Chương: Chương Al-Ma-idah
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại