Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Naba'   Câu:

Surat An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa makafiri ndio marejeo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Naba'
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại