《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 阿迪亚特   段:

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
阿拉伯语经注:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
阿拉伯语经注:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
阿拉伯语经注:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
阿拉伯语经注:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
阿拉伯语经注:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Na yeye ana pupa sana la mali.
阿拉伯语经注:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
阿拉伯语经注:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
阿拉伯语经注:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 阿迪亚特
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭