《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 拜莱德   段:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
阿拉伯语经注:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
阿拉伯语经注:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
阿拉伯语经注:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
阿拉伯语经注:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
阿拉伯语经注:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
阿拉伯语经注:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
阿拉伯语经注:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
阿拉伯语经注:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
阿拉伯语经注:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
阿拉伯语经注:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
阿拉伯语经注:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
阿拉伯语经注:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
阿拉伯语经注:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
阿拉伯语经注:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
au masikini asiyekuwa na kitu.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
阿拉伯语经注:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
阿拉伯语经注:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
阿拉伯语经注:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 拜莱德
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭