《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 莱仪拉   段:

Surat Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
阿拉伯语经注:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
阿拉伯语经注:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa kuumba mbea mbili: ya kiume na ya kike,
阿拉伯语经注:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
阿拉伯语经注:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
阿拉伯语经注:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
阿拉伯语经注:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
阿拉伯语经注:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
阿拉伯语经注:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
阿拉伯语经注:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamnyoshea njia za mateso.
阿拉伯语经注:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
阿拉伯语经注:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
阿拉伯语经注:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
阿拉伯语经注:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
阿拉伯语经注:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
阿拉伯语经注:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
kutoa Kwake si kwa kulipa zema alizofanyiwa na mtu.
阿拉伯语经注:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
阿拉伯语经注:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 莱仪拉
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭