《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 则里扎莱   段:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
阿拉伯语经注:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na ikatoa vilivyomo ndani yake: wafu na makandi.
阿拉伯语经注:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na akauliza binadamu, kwa babaiko, «Imezukiwa na nini?»
阿拉伯语经注:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku ya Kiyama ardhi itatoa habari ya mambo iliyofanyiwa ya uzuri na ubaya.
阿拉伯语经注:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameiamuru itoe habari ya mambo iliyofanyiwa.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo wataondoka kutoka kwenye kisimamo cha Hesabu wakiwa makundi, ili Mwenyezi Mungu Awaoneshe waliyoyatenda, mazuri na mabaya, na Awalipe kwayo.
阿拉伯语经注:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Yoyote mwenye kufanya jema wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
阿拉伯语经注:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na yoyote mwenye kufanya baya wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 则里扎莱
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭