Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Əli Muhsin Əl-Bervani * - Tərcumənin mündəricatı

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Mənaların tərcüməsi Ayə: (12) Surə: Hud
فَلَعَلَّكَ تَارِكُۢ بَعۡضَ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيۡكَ وَضَآئِقُۢ بِهِۦ صَدۡرُكَ أَن يَقُولُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ جَآءَ مَعَهُۥ مَلَكٌۚ إِنَّمَآ أَنتَ نَذِيرٞۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٌ
Basi labda utaacha baadhi ya yale yaliyo funuliwa kwako, na kifua kitaona dhiki kwa hayo, kwa sababu wanasema: Mbona hakuteremshiwa khazina, au wakaja naye Malaika? Wewe ni mwonyaji tu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wa kila kitu.
Ewe Nabii! Usijaribu kutaka kuwaridhi washirikina, kwani hao hawaamini. Na huenda ukijaribu kutaka kuwaridhi ukaacha kusoma baadhi ya uliyo letewa Wahyi, katika yale wasiyo penda wao kuyasikia, kama vile kudharauliwa baadhi ya miungu yao, kwa kukhofu kuwa wasije wakakejeli! Na huenda pengine ukahisi dhiki unapo wasomea, kwa kuwa wao wanataka Mwenyezi Mungu akuteremshie khazina ustarehe nayo kama wafalme, au waje nawe malaika watwambie ukweli wake! Basi, ewe Nabii! Usizibali inadi zao. Kwani wewe si chochote ila ni mwonyaji na mhadharishaji wa adhabu za Mwenyezi Mungu kwa anaye kwenda kinyume na amri yake. Nawe hayo umefanya, basi jipumzishe nafsi yako nao. Na jua kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuangalia na kulinda kila kitu. Naye atawafanyia kama wanavyo stahiki.
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Ayə: (12) Surə: Hud
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Əli Muhsin Əl-Bervani - Tərcumənin mündəricatı

Qurani Kərimin səvahili dilinə mənaca tərcüməsi. Tərcümə etdi: Əli Muhsin Əl-Bərvani.

Bağlamaq