Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Vers: (184) Surah / Kapitel: Al-Baqarah
أَيَّامٗا مَّعۡدُودَٰتٖۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۚ وَعَلَى ٱلَّذِينَ يُطِيقُونَهُۥ فِدۡيَةٞ طَعَامُ مِسۡكِينٖۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيۡرٗا فَهُوَ خَيۡرٞ لَّهُۥۚ وَأَن تَصُومُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Amewafaradhia Mwenyezi Mungu kufunga siku zinazojulikana idadi yake, nazo ni siku za mwezi wa Ramadhani. Basi yule kati yenu atakuwa mgonjwa, ikawa ni uzito kwake kufunga, au akawa ni msafiri, basi aweza kufungua. Na itamlazimu kufunga idadi ya siku nyengine zinazolingana na idadi ya siku alizokula. Na ni juu ya wale ambao kwao ni vigumu kufunga na ikawa inawaelemea maelemeo yasiyochukulika, kama mzee mkongwe na mngonjwa asiyetarajiwa kupoa, watoe fidiya ya kila siku ambayo watafungua, nayo ni kulisha masikini. Na yule atakayezidisha katika kiwango cha fidiya, kwa hiyari yake, basi hilo ni bora kwake. Na kufunga kwenu ni bora kwenu, pamoja na kuhimili shida, kuliko kutoa fidiya, iwapo mnazijua fadhila kubwa zipatikanazo kwenye kufunga mbele ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (184) Surah / Kapitel: Al-Baqarah
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen