Check out the new design

Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Anbiyāʾ   Vers:
قُلۡ إِنَّمَآ أُنذِرُكُم بِٱلۡوَحۡيِۚ وَلَا يَسۡمَعُ ٱلصُّمُّ ٱلدُّعَآءَ إِذَا مَا يُنذَرُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wale uliotumilizwa kwao, «Siwatishii adhabu ya Mwenyezi Mungu isipokuwa ni kwa wahyi wa Mwenyezi Mungu,» nao ni Qur’ani. «Lakini makafiri hawasikii yale wanayosomewa masikizi ya kuzingatia wanapoonya, na kwahivyo hawafaidiki nayo.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَلَئِن مَّسَّتۡهُمۡ نَفۡحَةٞ مِّنۡ عَذَابِ رَبِّكَ لَيَقُولُنَّ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Lau liliwapata makafiri fungu la adhabu ya Mwenyezi Mungu wangalijua mwisho wa kukanusha kwao na wangalilikabili hilo kwa kujiapiza maangamivu kwa sababu ya kujidhulumu kwao nafsi zao kwa kumuabudu kwao asiyekuwa Mwenyezi Mungu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَنَضَعُ ٱلۡمَوَٰزِينَ ٱلۡقِسۡطَ لِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَلَا تُظۡلَمُ نَفۡسٞ شَيۡـٔٗاۖ وَإِن كَانَ مِثۡقَالَ حَبَّةٖ مِّنۡ خَرۡدَلٍ أَتَيۡنَا بِهَاۗ وَكَفَىٰ بِنَا حَٰسِبِينَ
Na Mwenyezi Mungu Ataiweka Mizani ya uadilifu kwa ajili ya Hesabu katika siku ya Kiyama. Hawatadhulumiwa hawa wala wengine kitu chochote, hata kama ni kitendo, kizuri au kibaya, cha kadiri ya chungu mdogo, kitazingatiwa katika hesabu ya mwenyewe. Na inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyadhibiti matendo ya waja Wake na ni Mwenye kuwalipa kwayo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ ٱلۡفُرۡقَانَ وَضِيَآءٗ وَذِكۡرٗا لِّلۡمُتَّقِينَ
Kwa hakika, tulimpa Mūsā na Hārūn hoja na ushindi juu ya maadui wao na pia Kitabu, nacho ni Taurati, ambacho kwacho tumepambanua baina ya ukweli na urongo, na ambacho ni nuru ambayo kwayo wanajioongoza wachamungu wenye kuogopa adhabu ya Mola wao.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ٱلَّذِينَ يَخۡشَوۡنَ رَبَّهُم بِٱلۡغَيۡبِ وَهُم مِّنَ ٱلسَّاعَةِ مُشۡفِقُونَ
Na wao ni wenye kicho na hofu kwa kuuogopa wakati Kiyama kitasimama.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَهَٰذَا ذِكۡرٞ مُّبَارَكٌ أَنزَلۡنَٰهُۚ أَفَأَنتُمۡ لَهُۥ مُنكِرُونَ
Na hii Qur’ani ambayo Mwenyezi Mungu Ameiteremsha kwa Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukliye, ni ukumbusho kwa anayejikumbusha nayo na akatekeleza amri Zake na akajiepusha na makatazo Yake, ina kheri nyingi na manufaa makubwa. Je, mnaikanusha na hali ina upeo wa uwazi na ufunuzi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
۞ وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَآ إِبۡرَٰهِيمَ رُشۡدَهُۥ مِن قَبۡلُ وَكُنَّا بِهِۦ عَٰلِمِينَ
Kwa hakika, tulimpa Ibrāhīm uongofu wake ambao yeye aliwalingania watu waufuate kabla ya Mūsā na Hārūn. Na sisi tulikuwa tunajua kwamba yeye anastahiki hilo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا هَٰذِهِ ٱلتَّمَاثِيلُ ٱلَّتِيٓ أَنتُمۡ لَهَا عَٰكِفُونَ
Pindi aliposema kumwambia babake na watu wake, «Ni masanamu gani hawa mliowatengeneza kisha mkakaa kuwaabudu na mkajilazimisha nao.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قَالُواْ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا لَهَا عَٰبِدِينَ
Wakasema, «Tuliwapata baba zetu wakiwaabudu, na sisi tunawaabudu kwa kuwaiga wao.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قَالَ لَقَدۡ كُنتُمۡ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمۡ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Ibrāhīm akawaambia, «Kwa hakika nyinyi na wazee wenu, kwa kukuwaabudu kwenu hawa masanamu, muko mbali waziwazi na haki.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قَالُوٓاْ أَجِئۡتَنَا بِٱلۡحَقِّ أَمۡ أَنتَ مِنَ ٱللَّٰعِبِينَ
Wakasema, «Je, neno hili ambalo umekuja nalo kwetu ni la usawa na ukweli, au neno lako ni la mtu anayefanya mzaha na shere, hajui analosema?»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قَالَ بَل رَّبُّكُمۡ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ ٱلَّذِي فَطَرَهُنَّ وَأَنَا۠ عَلَىٰ ذَٰلِكُم مِّنَ ٱلشَّٰهِدِينَ
Ibrāhīm, rehema na amani zimshukie, akasema, «Bali Mola wenu Ambaye ninawalingania mumuabudu Ndiye Mola wa mbingu na ardhi Ambaye Ameziumba, na mimi ni mwenye kulitolea ushahidi hilo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَتَٱللَّهِ لَأَكِيدَنَّ أَصۡنَٰمَكُم بَعۡدَ أَن تُوَلُّواْ مُدۡبِرِينَ
«Na ninaapa kwa Mwenyezi Mungu, nitawachimba masanamu wenu niwavunjevunje baada ya nyinyi kuondoka kwenda zenu na kuwaacha.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Anbiyāʾ
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Übersetzungen

Übersetzt von Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr und Scheich Nasser Khamis.

Schließen