Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Vers: (112) Surah / Kapitel: Al -I-‘Imrân
ضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ أَيۡنَ مَا ثُقِفُوٓاْ إِلَّا بِحَبۡلٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَحَبۡلٖ مِّنَ ٱلنَّاسِ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَسۡكَنَةُۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ
Amejaalia Mwenyezi Mungu utwevu na unyonge kuwa ni jambo lenye kuambatana nao Mayahudi na wala haliwaepuki. Kwa hivyo, wao daima ni madhalili wenye kudharauliwa popote waliopo, isipokuwa watakapokuwa na mafungamano na Mwenyezi Mungu na makubaliano na watu ambayo kwayo watajiwekea usalama wa nafsi zao na mali zao. Hayo ndiyo mapatano ya kujidhamini kwao na kujilazimisha kwao kufuata hukumu za Uislamu. Na wamerudi nyuma wakiwa wamepata hasira za Mwenyezi Mungu zilizowastahili. Na wamepigwa na unyonge na umasikini. Kwa hivyo, humuoni Myahudi isipokuwa utamkuta ameshukiwa na hofu na babaiko kwa kuwaogopa Waumini. Hilo ndilo Alilowajaalia Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kumkufuru kwao Mwenyezi Mungu, kukeuka kwao mipaka Yake na kuwaua kwao Manabii, kwa udhalimu na uonevu. Na hakuna lolote lililowafanya wao wawe majasiri wa kuyatenda haya isipokuwa ni kule kufanya kwao maasia na kukiuka kwao mipaka ya Mwenyezi Mungu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (112) Surah / Kapitel: Al -I-‘Imrân
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen