Check out the new design

Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Ar-Rūm   Vers:

Ar-Rum

الٓمٓ
«Alif, Lām, Mīm» Yametangulia maelezo kuhusu herufi zilizokatwa- katwa na kutengwa mwanzo wa sura ya Al-Baqarah.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
غُلِبَتِ ٱلرُّومُ
Wafursi waliwashinda Warumi
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فِيٓ أَدۡنَى ٱلۡأَرۡضِ وَهُم مِّنۢ بَعۡدِ غَلَبِهِمۡ سَيَغۡلِبُونَ
katika sehemu za karibu za ardhi ya Shamu kuelekea Uajemi. Na Warumi watawashinda Wafursi
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فِي بِضۡعِ سِنِينَۗ لِلَّهِ ٱلۡأَمۡرُ مِن قَبۡلُ وَمِنۢ بَعۡدُۚ وَيَوۡمَئِذٖ يَفۡرَحُ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
katika kipindi kisichopita miaka kumi na kisichopungua miaka mitatu. Ni ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, amri yote kabla ya ushindi wa Warumi na baada yake. Na siku hiyo ambayo Warumi watapata ushindi juu ya Wafursi Waumini wataifurahia nusura ya Mwenyezi Mungu kwa Warumi juu ya Wafursi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
بِنَصۡرِ ٱللَّهِۚ يَنصُرُ مَن يَشَآءُۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na Mwenyezi Mungu, Kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Anamsaidia Anayemtaka na Anaacha kumsaidia Anayemtaka. Na Yeye Ndiye Mshindi Ambaye hakuna wa kushindana naye, Ndiye Mwenye kumrehemu Anayemtaka miongoni mwa viumbe Vyake. Na hilo lilithibitika, na Warumi waliwashinda Wafursi baada ya miaka saba, na Waislamu wakafurahi kwa hilo, kwa kuwa Warumi walikuwa ni watu wa Kitabu ingawa wamekipotosha.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Ar-Rūm
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Übersetzungen

Übersetzt von Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr und Scheich Nasser Khamis.

Schließen