Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Vers: (94) Surah / Kapitel: Al-Mâ’ida
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَيَبۡلُوَنَّكُمُ ٱللَّهُ بِشَيۡءٖ مِّنَ ٱلصَّيۡدِ تَنَالُهُۥٓ أَيۡدِيكُمۡ وَرِمَاحُكُمۡ لِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ مَن يَخَافُهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ فَمَنِ ٱعۡتَدَىٰ بَعۡدَ ذَٰلِكَ فَلَهُۥ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, Mwenyezi Mungu Atawapa mtihani wa baadhi ya viwindwa vya barani, watakaokuja karibu na nyinyi kwa namna isiyo ya kawaida muweze kuwashika wadogo wao bila kutumia silaha na kuwashika wakubwa wao kwa kutumia silaha, ili Mwenyezi Mungu Awajue, ujuzi uliyofunuka wazi kwa viumbe, wale wanaomuogopa Mola wao kwa ghaibu kwa kuwa wana yakini kuwa ujuzi wa Mwenyezi Mungu kuhusu wao umekamilika, na kwa hivyo waache kuwinda wakiwa katika hali ya ihram (ihramu: kuingia kwenye ibada ya Hija au Umra). Basi yoyote mwenye kuvuka mpaka wake, baada ya maelezo haya, akafanya ujasiri wa kuwinda, na hali yeye yuko kwenye ihramu, anastahili adhabu kali.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (94) Surah / Kapitel: Al-Mâ’ida
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen