Check out the new design

Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Mujādilah   Vers:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۖ مَا يَكُونُ مِن نَّجۡوَىٰ ثَلَٰثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمۡ وَلَا خَمۡسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمۡ وَلَآ أَدۡنَىٰ مِن ذَٰلِكَ وَلَآ أَكۡثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمۡ أَيۡنَ مَا كَانُواْۖ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُواْ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ
Kwani hujui kwamba Mwenyezi Mungu Yuwajua kila kitu kilicho mbinguni na ardhini? Hawanong’oni watu watatu, kati ya viumbe Vyake, maneno ya siri isipokuwa Mwenyezi Mungu ni wanne wao , wala watano isipokuwa Yeye ni wa sita wao, wala wachache kuliko idadi hiyo iliyotajwa wala wengi kuliko idadi hiyo isipokuwa Yeye Huwa Yuko pamoja nao kwa ujuzi wake, mahali popote waliopo. Hakuna chochote kinachofichamana Kwake kuhusu mambo yao. Kisha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Siku ya Kiyama, Atawapa habari ya kile walichokifanya chema au kibaya na Atawalipa kwa walichokifanya. Hakika Mwenyezi Mungu kwa kila kitu ni Mjuzi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ نُهُواْ عَنِ ٱلنَّجۡوَىٰ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَيَتَنَٰجَوۡنَ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِۖ وَإِذَا جَآءُوكَ حَيَّوۡكَ بِمَا لَمۡ يُحَيِّكَ بِهِ ٱللَّهُ وَيَقُولُونَ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ لَوۡلَا يُعَذِّبُنَا ٱللَّهُ بِمَا نَقُولُۚ حَسۡبُهُمۡ جَهَنَّمُ يَصۡلَوۡنَهَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Je, huwaoni, ewe Mtume, Mayahudi waliokatazwa wasizungumze kwa siri maneno yanayowatia shaka Waumini, kisha wanarudi kufanya yale waliyokatazwa, na wanazungumza kwa siri maneno ya dhambi, uadui na kuenda kinyume na amri ya Mtume? Na wanapokujia hawa Mayahudi kwa jambo lolote miongoni mwa mambo, wanakuamkia kwa maamkizi ambayo siyo yale Mwenyezi Mungu Aliyoyafanya ni maamkizi yako, na wanasema, «As-sām ‘alayka» yaani, Mauti yakushukie! Na wanasema wakiambiana wao kwa wao, «Si Atuangamize Mwenyezi Mungu kwa yale tunayomuambia Muhammad, iwapo ni Mtume kikweli.» Moto wa Jahanamu utawatosha: wataungia na watalihisi joto lake, na ubaya wa marejeo ni huo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَنَٰجَيۡتُمۡ فَلَا تَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِ وَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡبِرِّ وَٱلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Mnapozungumza baina yenu kwa siri, msizungumze maneno ya dhambi au yenye uadui kwa wengine msiokuwa nyinyi au yanayoenda kinyume na amri ya Mtume. Na zungumzeni yale yenye kheri, utiifu na wema, na muogopeni Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake, Kwani Kwake Yeye Peke Yake ndipo mtakaporudi na matendo yenu yote na maneno yenu Aliyowadhibitia, na Atawalipa kwayo.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِنَّمَا ٱلنَّجۡوَىٰ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ لِيَحۡزُنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَيۡسَ بِضَآرِّهِمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Hakika kuzungumza kwa siri maneno ya dhambi na uadui ni katika ushawishi wa Shetani. Yeye ndiye anayeyapamba na kuyahimiza ili atie masikitiko kwenye nyoyo za Waumini. Na hilo halikuwa ni lenye kuwaudhi Waumini kitu chochote isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na mapendeleo Yake. Na kwa Mwenyezi Mungu na wajitegemeze wenye kumuamini katika mambo yao yote.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَكُمۡ تَفَسَّحُواْ فِي ٱلۡمَجَٰلِسِ فَٱفۡسَحُواْ يَفۡسَحِ ٱللَّهُ لَكُمۡۖ وَإِذَا قِيلَ ٱنشُزُواْ فَٱنشُزُواْ يَرۡفَعِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنكُمۡ وَٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ دَرَجَٰتٖۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Mkitakiwa mpanane nafasi kwenye mabaraza basi peaneni nafasi, na mkifanya hivyo Mwenyezi Mungu Atawakunjulia nafasi duniani na Akhera. Na mkitakiwa kwenu, enyi Waumini, muinuke katika mabaraza yenu kwa jambo lolote lenye kheri kwenu, basi inukeni. Mwenyezi Mungu Anavipandisha vyeo vya Waumini miongoni mwenu, na Anavipandisha vyeo vya wenye elimu daraja nyingi kwa kuwapatia malipo mema na daraja za kupata radhi. Na Mwenyezi Mungu Anayatambua matendo yenu, hakuna chochote kinachofichamana Kwake katika hayo, na Yeye ni mwenye kuwalipa nyinyi kwayo. Katika aya pana kutukuza cheo cha wanavyuoni na utukufu wao na kutukuzwa daraja zao.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Mujādilah
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Übersetzungen

Übersetzt von Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr und Scheich Nasser Khamis.

Schließen