Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Übersetzungen

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Übersetzung der Bedeutungen Vers: (115) Surah / Kapitel: An-Nahl
إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةَ وَٱلدَّمَ وَلَحۡمَ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦۖ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Amekuharimishieni nyamafu tu, na damu, na nyama ya nguruwe,na mnyama aliye chinjwa kwa ajili isiyo kuwa ya Mwenyezi Mungu. Lakini anaye lazimishwa bila ya kuasi, wala kuruka mipaka, basi hakika MwenyeziMungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.
Kwani hakika Mwenyezi Mungu hakukuharimishieni isipo kuwa nyamafu, na damu inayo tiririka kutokana na mnyama wakati wa kumchinja, na nyama ya nguruwe, na kilicho chinjwa kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu. Lakini mwenye kulazimishwa na shida ya njaa kula kitu alicho kuharimishieni Mwenyezi Mungu, bila ya kutaka, na wala bila ya kupita hadi ya kiasi cha kuondoa ile dharura, basi hakika Mwenyezi Mungu hayachukulii hayo. Kwani Yeye Subhanahu ni Mwenye kuwasamehe waja wake. Huwasamehe wanapo tumbukia katika makosa wasio endelea nayo. Naye ni Mwenye kuwarehemu kwa vile anawazuia vitu vinavyo wadhuru, na anawaruhusu kwa kuhifadhi uhai wao.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (115) Surah / Kapitel: An-Nahl
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Schließen