Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Übersetzungen

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Übersetzung der Bedeutungen Vers: (77) Surah / Kapitel: An-Nisâ’
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ قِيلَ لَهُمۡ كُفُّوٓاْ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقِتَالُ إِذَا فَرِيقٞ مِّنۡهُمۡ يَخۡشَوۡنَ ٱلنَّاسَ كَخَشۡيَةِ ٱللَّهِ أَوۡ أَشَدَّ خَشۡيَةٗۚ وَقَالُواْ رَبَّنَا لِمَ كَتَبۡتَ عَلَيۡنَا ٱلۡقِتَالَ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنَآ إِلَىٰٓ أَجَلٖ قَرِيبٖۗ قُلۡ مَتَٰعُ ٱلدُّنۡيَا قَلِيلٞ وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّمَنِ ٱتَّقَىٰ وَلَا تُظۡلَمُونَ فَتِيلًا
Je, huwaoni wale walio ambiwa: Izuieni mikono yenu, na mshike Swala na mtoe Zaka. Na walipo amrishwa kupigana, mara kundi moja kati yao liliwaogopa watu kama kumwogopa Mwenyezi Mungu, au kwa khofu kubwa zaidi. Na wakasema: Mola Mlezi wetu! Kwa nini umetuamrisha kupigana? Laiti unge tuakhirishia kiasi ya muda kidogo hivi! Sema: Starehe ya dunia ni ndogo, na Akhera ni bora zaidi kwa mwenye kuchamngu. Wala hamtadhulumiwa hata uzi wa kokwa ya tende.
Ewe Muhammad! Hebu huwaangalii ukawastaajabia wale walio taka kupigana kabla ya kuja ruhusa, wakaambiwa: Bado haujafika wakati wa vita. Basi izuieni mikono yenu msipigane. Bali shughulikieni kushika Swala, na kutoa Zaka. Na Mwenyezi Mungu alipo waamrisha wapigane kikawa kikundi kimoja kati yao kikawa kinawaogopa watu kama kumkhofu Mwenyezi Mungu, au zaidi. Wakasema kwa kuona ni mageni hayo: Kwa nini ukatuamrisha kupigana? Wao walidhani kuwa kuamrishwa vita kunahimiza ajali yao, na kwa hivyo wakasema: Hebu lau ungeli tungojea muda kidogo tupate kustarehe na ulimwengu! Waambie: Songeni mbele mkapigane hata ikiwa mtakufa mashahidi, kwani starehe ya dunia, ingawa ni kubwa vipi, ni chache ukilinganisha na starehe ya Akhera. Na Akhera ni bora na kubwa zaidi kwa mwenye kumcha Mwenyezi Mungu, na huko mtakuja lipwa kwa vitendo vyenu vya duniani, wala hampunguziwi hata chembe katika ujira wenu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Vers: (77) Surah / Kapitel: An-Nisâ’
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Schließen