Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (54) Sura: Suratu Houd
إِن نَّقُولُ إِلَّا ٱعۡتَرَىٰكَ بَعۡضُ ءَالِهَتِنَا بِسُوٓءٖۗ قَالَ إِنِّيٓ أُشۡهِدُ ٱللَّهَ وَٱشۡهَدُوٓاْ أَنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ
Sisi tunasema: Baadhi katika miungu yetu imekusibu kwa baa. Akasema: Hakika mimi namshuhudisha Mwenyezi Mungu, na nyinyi shuhudieni, ya kwamba mimi najitenga mbali na hao mnao wafanya washirika,
Na hatuna la kusema juu ya msimamo wako nasi ila kuwa mmojapo katika miungu yetu imekupatiliza kwa shari, ndio maana ukawa unaropokwa maneno haya! Naye akasema naye ameshikilia Imani yake na anawapinga: Ninasema, na namshuhudisha Mwenyezi Mungu kwa haya niyasemayo, na nakushuhudisheni nyinyi, ya kwamba mimi najitenga mbali kabisa na maradhi ya ushirikina mliyo nayo. Kwani nyinyi ni wagonjwa!
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (54) Sura: Suratu Houd
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa