Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (60) Sura: Suratu Houd
وَأُتۡبِعُواْ فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا لَعۡنَةٗ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ أَلَآ إِنَّ عَادٗا كَفَرُواْ رَبَّهُمۡۗ أَلَا بُعۡدٗا لِّعَادٖ قَوۡمِ هُودٖ
Na wakafuatishiwa laana katika dunia hii na Siku ya Kiyama. Basi tambueni mtanabahi! Hakika kina A'adi walimkufuru Mola wao Mlezi. Na tambueni mtanabahi kuwa hakika waliangamizwa kina A'adi, kaumu ya Huud.
Kwa hivyo wakastahiki kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na Malaika, na watu wote kupata laana ya hapa duniani, na laana ya kuwafuatia Siku ya Kiyama. Basi na atanabahi kila mwenye kuijua khabari ya A'adi kwamba hao kina A'adi waliikataa neema ya Muumba wao kwao, wala hawakuishukuru kwa kumuamini Yeye peke yake. Kwa hivyo ndio wakawa wanastahili wafukuzwe kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu, na wateremshiwe maangamizo makali! Hebu zingatieni maangamizo yao kwa kumkadhibisha Huud!
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (60) Sura: Suratu Houd
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa