Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (63) Sura: Suratu Houd
قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَءَاتَىٰنِي مِنۡهُ رَحۡمَةٗ فَمَن يَنصُرُنِي مِنَ ٱللَّهِ إِنۡ عَصَيۡتُهُۥۖ فَمَا تَزِيدُونَنِي غَيۡرَ تَخۡسِيرٖ
Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa ninazo dalili zilizo wazi kutokana na Mola wangu Mlezi, naye akawa kanipa rehema kutoka kwake - je, ni nani atakaye ninusuru kwa Mwenyezi Mungu nikimuasi? Basi nyinyi hamtanizidishia ila khasara tu.
Akasema: Enyi watu wangu! Hebu nambieni: ikiwa mimi kwa haya ninayo kukuitieni kwayo nina ujuzi nayo vilivyo, na nina hoja za kunitia nguvu kutoka kwa Mola wangu Mlezi, na ikawa Mola wangu Mlezi kanipa mimi na nyinyi rehema itokayo kwake, nayo ni Unabii na Utume, vipi basi nende kinyume na amri yake, na nimuasi kwa kutofikisha ujumbe wake kwa sababu ya kukusikilizeni nyinyi? Na nani wa kuninusuru na kunisaidia kuikinga adhabu yake nikimuasi Yeye? Nyinyi hamwezi kuninusuru na kunikinga na adhabu yake. Basi hamtonizidishia ila kupotea na kuingia khasarani ni kikut'iini nyinyi, na nikamuasi Mola wangu na Mola wenu Mlezi.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (63) Sura: Suratu Houd
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa