Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (33) Sura: Suratu Al'nahl
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ أَوۡ يَأۡتِيَ أَمۡرُ رَبِّكَۚ كَذَٰلِكَ فَعَلَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ وَمَا ظَلَمَهُمُ ٱللَّهُ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ
Wanangojea jengine hawa ila Malaika wawafikie, au iwafikie amri ya Mola wako Mlezi? Kama hivyo walitenda walio kuwa kabla yao. Na MwenyeziMungu hakuwadhulumu, lakini walijidhulumu wenyewe.
Hao ndio wachamngu walio jitengenezea Akhera yao. Na hayo ndiyo malipo yao. Ama washirikina kwa sababu ya inadi yao na kubakia kwao kwenye ushirikina wao, hawataraji ila Malaika waje kunyakua roho zao nao wamezidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na vitendo vya shari. Na itawajia adhabu ya Mola wako Mlezi iwateketeze wote. Na kama walivyo fanya makafiri hawa, basi walikwisha wafanyia Manabii wao wale walio watangulia, na Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa vitendo vyao. Wala Yeye hakuwadhulumu pale alipo waadhibu, lakini wao wenyewe walizidhulumu nafsi zao walipo zitia katika adhabu kwa ukafiri wao.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (33) Sura: Suratu Al'nahl
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa