Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (1) Sura: Suratu Al'ma'ida

Surat Al-Ma'idah

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَوۡفُواْ بِٱلۡعُقُودِۚ أُحِلَّتۡ لَكُم بَهِيمَةُ ٱلۡأَنۡعَٰمِ إِلَّا مَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ غَيۡرَ مُحِلِّي ٱلصَّيۡدِ وَأَنتُمۡ حُرُمٌۗ إِنَّ ٱللَّهَ يَحۡكُمُ مَا يُرِيدُ
Enyi mlio amini! Timizeni ahadi. Mmehalalishiwa wanyama wa mifugo, ila wale mnao tajiwa. Lakini msihalalishe kuwinda nanyi mmo katika Hija. Hakika Mwenyezi Mungu anahukumu apendavyo.
Enyi Waumini! Jilazimisheni kutimiza ahadi zote baina yenu na Mwenyezi Mungu, na ahadi za kisharia zilio baina yenu na watu wengineo. Na Mwenyezi Mungu amekuhalalishieni kula nyama howa, yaani nyama wa kufuga, kama ngamia, ng'ombe, kondoo, mbuzi n.k. ila wale mlio tajiwa kuwa ni haramu. Wala haikujuzieni kuwinda barani pale mnapo kuwa mmeharimia Hija, au mpo katika eneo la ardhi takatifu. Hakika Mwenyezi Mungu huhukumu apendavyo kwa hikima yake. Yeye ndiye Muumbaji, na ndiye Mwenye kujua jema na baya la viumbe vyake. Na haya ni miongoni mwa ahadi za Mwenyezi Mungu zilio juu yenu.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (1) Sura: Suratu Al'ma'ida
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa