Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Aya: (43) Sura: Suratu Al'anfal
إِذۡ يُرِيكَهُمُ ٱللَّهُ فِي مَنَامِكَ قَلِيلٗاۖ وَلَوۡ أَرَىٰكَهُمۡ كَثِيرٗا لَّفَشِلۡتُمۡ وَلَتَنَٰزَعۡتُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ سَلَّمَۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Kumbuka alipo kuonyesha usingizini mwako kwamba wao ni wachache - na lau angeli kuonyesha kuwa ni wengi, mngeli ingiwa na woga, na mngeli zozana katika jambo hilo. Lakini Mwenyezi Mungu kakuvueni. Hakika Yeye ni Mwenye kuyajua yalio vifuani.
Na kumbuka, ewe Mtume! Pale Mwenyezi Mungu alipo kufadhili kwa kukuonyesha usingizini ndoto ya kuwa hilo jeshi la maadui ni dogo, ili akutulizeni nyoyo muamini kuwa mtawashinda, kwa hivyo muwe imara kuwakaabili. Na lau angeli kuacheni muwaone wengi, bila ya kukuthibitisheni kwa ndoto hiyo, mngeli waogopa, na mkasita sita kupigana nao, na mngeli emewa, na mkazozana msonge mbele au mrudi. Lakini Mwenyezi Mungu amekuvueni na hayo, na akakuokoeni na matokeo yake, kwani hakika Yeye ni Mwenye kuyajua vyema yaliyomo ndani ya vifua vya watu.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (43) Sura: Suratu Al'anfal
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Rufewa