Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'burouj   Aya:

Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Ninaapa kwa mbingu yenye nyota kubwa kubwa!
Tafsiran larabci:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa siku iliyoahidiwa!
Tafsiran larabci:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi na kinachoshuhudiwa!
Tafsiran larabci:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wameangamizwa watu wa makhandaki.
Tafsiran larabci:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Yenye moto wenye kuni nyingi.
Tafsiran larabci:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Walipokuwa wamekaa hapo.
Tafsiran larabci:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Na wao ni mashahidi wa yale waliyokuwa wakiwafanyia Waumini.
Tafsiran larabci:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa.
Tafsiran larabci:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shahidi wa kila kitu.
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika waliowafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Hakika walioamini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Tafsiran larabci:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
Tafsiran larabci:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Yeye ndiye anayeanzisha na ndiye anayerejesha tena.
Tafsiran larabci:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi.
Tafsiran larabci:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu.
Tafsiran larabci:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Atendaye ayatakayo.
Tafsiran larabci:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je! Zimekuwasilia habari za majeshi?
Tafsiran larabci:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Ya Firauni na Thamudi?
Tafsiran larabci:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Lakini waliokufuru wamo katika kukadhibisha.
Tafsiran larabci:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazingira.
Tafsiran larabci:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur-ani tukufu.
Tafsiran larabci:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
Katika Ubao Uliohifadhiwa.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'burouj
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Wani gungu na cibiyar fassara ta Ruwad ne suka fassarasu tare da haɗin gwiwar Ƙungiyar Da'awa ta Rabwah da Kungiyar hidimtawa abinda Musulunci ya kunsa da yaruka

Rufewa