Check out the new design

Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dilinde Tercüme - Abdullah Muhammed ve Nasır Hamiys * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûratu's-Sebe   Ayet:
وَيَوۡمَ يَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ يَقُولُ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ أَهَٰٓؤُلَآءِ إِيَّاكُمۡ كَانُواْ يَعۡبُدُونَ
Kumbuka, ewe Mtume, Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atawafufua washirikina na waabudiwa badala Yake miongoni mwa Malaika, kisha Awaambie Malaika kwa njia ya kuwalaumu wale waliowaabudu, «Je ni hawa waliokuwa wakiwaabudu badala yetu sisi?»
Arapça tefsirler:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَكَ أَنتَ وَلِيُّنَا مِن دُونِهِمۖ بَلۡ كَانُواْ يَعۡبُدُونَ ٱلۡجِنَّۖ أَكۡثَرُهُم بِهِم مُّؤۡمِنُونَ
Malaika watasema, «Tunakutakasa, ewe Mwenyezi Mungu, na kuwa na mshirika wa kuabudiwa! wewe Ndiye Msimamizi wetu tunayemtii na kumuabudu Peke Yake. Bali hawa walikuwa wakiwaabudu mashetani, wengi wao wanawaamini na kuwatii.»
Arapça tefsirler:
فَٱلۡيَوۡمَ لَا يَمۡلِكُ بَعۡضُكُمۡ لِبَعۡضٖ نَّفۡعٗا وَلَا ضَرّٗا وَنَقُولُ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلنَّارِ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
Basi Siku ya Ufufuzi, hao waabudiwa hawatakuwa na mamlaka ya kuwanufaisha au kuwadhuru wenye kuwaabudu. Na tutasema kuwaambia wale waliozidhulumu nafsi zao, «Onjeni adhabu ya Moto ambao mlikuwa mkiukanusha!»
Arapça tefsirler:
وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُنَا بَيِّنَٰتٖ قَالُواْ مَا هَٰذَآ إِلَّا رَجُلٞ يُرِيدُ أَن يَصُدَّكُمۡ عَمَّا كَانَ يَعۡبُدُ ءَابَآؤُكُمۡ وَقَالُواْ مَا هَٰذَآ إِلَّآ إِفۡكٞ مُّفۡتَرٗىۚ وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ
Na wanaposomewa makafiri wa Makkah aya za Mwenyezi Mungu zikiwa wazi wao wanasema, «Hakuwa Muhammad isipokuwa ni mtu anayependa kuwakataza nyinyi kuwaabudu waungu ambao baba zenu walikuwa wakiwaabudu,» na wanasema, «Haikuwa hii Qur’ani isipokuwa ni urongo uliozuliwa, umeuleta wewe mwenyewe na sio kuwa unatoka kwa Mwenyezi Mungu.» Na makafiri walisema kuhusu Qur’ani ilipowajia, «Haikuwa hii isipokuwa uchawi uliojitokeza wazi.»
Arapça tefsirler:
وَمَآ ءَاتَيۡنَٰهُم مِّن كُتُبٖ يَدۡرُسُونَهَاۖ وَمَآ أَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمۡ قَبۡلَكَ مِن نَّذِيرٖ
Na hatukuwateremshia wakanushaji vitabu vya wao kuvisoma kabla ya Qur’ani vikawa vitawaonyesha wao yale wanayoyadai kwamba kile alichokuja nacho Muhammad ni uchawi, na hatukumtuma kwao kabla yako wewe, mjumbe yoyote wa kuwaonya wao adhabu yetu.
Arapça tefsirler:
وَكَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ وَمَا بَلَغُواْ مِعۡشَارَ مَآ ءَاتَيۡنَٰهُمۡ فَكَذَّبُواْ رُسُلِيۖ فَكَيۡفَ كَانَ نَكِيرِ
Na walikanusha wale waliokuwa kabla yao, kama vile 'Ād na Thamūd, Na watu wa Makkah hawakufikia ushuri wa kile tulichowapa ummah waliopita cha nguvu, wingi wa mali, umri mrefu na neema nyiginezo, na tukawaangamiza. Basi angalia, ewe Mtume! Ni namna gani yalivyokuwa makemeo yangu na adhabu yangu kwao?
Arapça tefsirler:
۞ قُلۡ إِنَّمَآ أَعِظُكُم بِوَٰحِدَةٍۖ أَن تَقُومُواْ لِلَّهِ مَثۡنَىٰ وَفُرَٰدَىٰ ثُمَّ تَتَفَكَّرُواْۚ مَا بِصَاحِبِكُم مِّن جِنَّةٍۚ إِنۡ هُوَ إِلَّا نَذِيرٞ لَّكُم بَيۡنَ يَدَيۡ عَذَابٖ شَدِيدٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie hawa wakanushaji washindani, «Mimi ninawapa ushauri mmoja: msimame kumtii Mwenyezi Mungu wawili-wawili na mmoja-mmoja, kisha mfikirie kuhusu hali ya mwenzenu, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kile alichonasibishwa nacho. Yeye hana wazimu. Hakuwa Yeye isipokuwa ni mwenye kuwatisha na kuwaonya adhabu ya Jahanamu kabla joto lake halijawasumbua.»
Arapça tefsirler:
قُلۡ مَا سَأَلۡتُكُم مِّنۡ أَجۡرٖ فَهُوَ لَكُمۡۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٞ
Sema, ewe Mtume, uwaambie wakanushaji, «Malipo niliyowaomba kwa wema huu niliowaletea ni yenu nyinyi. Malipo yangu mimi ninayoyangojea hayapo isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu Mwenye kuyaona matendo yangu na matendo yenu.Hakuna chochote kinachofichamana Kwake. Yeye Anawalipa wote: kila mmoja kwa anachostahiki.»
Arapça tefsirler:
قُلۡ إِنَّ رَبِّي يَقۡذِفُ بِٱلۡحَقِّ عَلَّٰمُ ٱلۡغُيُوبِ
Sema, ewe Mtume, umwambie anayekanusha upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na ujumbe wa Uislamu, «Hakika Mola wangu Anauvurumiza ubatilifu kwa hoja za ukweli, hivyo basi ukaufedhehi na ukauangamiza. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mno wa vitu visivyoonekana, hakuna kinachofichamana Kwake chochote ardhini na mbinguni.»
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûratu's-Sebe
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dilinde Tercüme - Abdullah Muhammed ve Nasır Hamiys - Mealler fihristi

Dr. Abdullah Muhammed Abubekir ve Şeyh Nasır Hamis tarafından tercüme edilmiştir.

Kapat