Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Ayet: (16) Sure: Sûratu Yûnus
قُل لَّوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا تَلَوۡتُهُۥ عَلَيۡكُمۡ وَلَآ أَدۡرَىٰكُم بِهِۦۖ فَقَدۡ لَبِثۡتُ فِيكُمۡ عُمُرٗا مِّن قَبۡلِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Sema: Mwenyezi Mungu angeli taka nisingeli kusomeeni, wala nisingeli kujuvyeni. Kwani nalikwisha kaa nanyi umri mzima kabla yake! Basi, je! Hamzingatii?
Waambie ewe Mtume! Lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka kuwa asiniteremshie Qur'ani kutoka kwake, wala mimi nisikufikishieni, asingeli teremsha, wala mimi nisingeli kusomeeni, na wala Mwenyezi Mungu asingeli kufundisheni. Lakini Yeye kateremsha, na kanituma mimi kwayo, na mimi nimekusomeeni kama alivyo niamrisha. Na mimi nilikwisha kaa nanyi wakati mrefu kabla ya kupewa Utume, na mimi sikudai Utume wakati huo, wala sikukusomeeni kitu chochote. Na nyinyi mmeshuhudia kuwa mimi ni mkweli na muaminifu. Lakini umekuja Ufunuo na nimeamrishwa niusome. Basi hebu yatieni akilini haya mambo, na myazingatie, na yakutanisheni yaliyo pita ya zamani na ya yaliopo sasa.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Ayet: (16) Sure: Sûratu Yûnus
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat