Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Ayet: (1) Sure: Sûratu Hûd

Surat Hud

الٓرۚ كِتَٰبٌ أُحۡكِمَتۡ ءَايَٰتُهُۥ ثُمَّ فُصِّلَتۡ مِن لَّدُنۡ حَكِيمٍ خَبِيرٍ
Alif Lam Ra. Hiki ni Kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi, kisha zikapambanuliwa, kilicho toka kwa Mwenye Hikima na Mwenye Khabari!
Alif Lam Ra (A.L.R.)...Hizi ni harufi zilizo anziwa Sura hii kuwa ni ishara kuwa Qur'ani ni muujiza juu ya kuwa imeundwa kwa hizi hizi harufi zinazo tamkwa, na pia ni kuwazindua watu wanapo isikiliza inapo somwa Qur'ani Tukufu kuwa ni Kitabu chenye shani kuu. Zimeteremshwa Aya zake zimeshikana, madhubuti, hazina ndani yake upotovu, wala ubabaishi, na zimetungwa kwa njia isiyo na dosari, iwazi, na yenye kubainisha. Kisha hukumu zake zikapambanuliwa. Na Kitabu hichi juu ya utukufu wake ulio nao nafsi yake, kina utukufu zaidi kwa kuwa kimetokana na Mwenyezi Mungu ambaye anajua kila kitu, na Yeye Subhanahu anapanga mambo yote kwa pahala pake.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Ayet: (1) Sure: Sûratu Hûd
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat