قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى


مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (42) سۈرە: سۈرە ئەنپال
إِذۡ أَنتُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلدُّنۡيَا وَهُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلۡقُصۡوَىٰ وَٱلرَّكۡبُ أَسۡفَلَ مِنكُمۡۚ وَلَوۡ تَوَاعَدتُّمۡ لَٱخۡتَلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡمِيعَٰدِ وَلَٰكِن لِّيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗا لِّيَهۡلِكَ مَنۡ هَلَكَ عَنۢ بَيِّنَةٖ وَيَحۡيَىٰ مَنۡ حَيَّ عَنۢ بَيِّنَةٖۗ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَسَمِيعٌ عَلِيمٌ
Na kumbukeni pindi mlipokuwa kwenye upande wa bonde lililokuwa karibu sana na mji wa Madina na maadui zenu wameshukia kwenye upande wa bonde la mbali, na msafara wa biashara upande wenu wa chini unaelekea kwenye ufuo wa Bahari Nyekundu. Na lau kama mungalijaribu kuweka maelewano ya makutano hayo mungalitafautiana, lakini Mwenyezi Mungu Aliwakusanya bila kuagana ili Alipitishe jambo ambalo ililazimu lifanyike kwa kuwaokoa vipenzi Vyake na kuwadhalilisha maadui Wake kwa kuuawa na kushikwa mateka. Na hili lilifanyika ili apate kuangamia mwenye kuangamia kati yao kutokamana na hoja ya Mwenyezi Mungu iliyomthibitikia akaiyona na ikaondoa udhuru wake, na apate kuishi mwenye kuishi kutokamana na hoja ya Mwenyezi Mungu iliyomthibitikia na kujitokeza wazi kwake. Na kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasikia maneno ya makundi mawili hayo, hakifichiki Kwake chochote, ni Menye kuzijua nia zao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (42) سۈرە: سۈرە ئەنپال
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

تاقاش