قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (258) سۈرە: سۈرە بەقەرە
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِي حَآجَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ فِي رَبِّهِۦٓ أَنۡ ءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ إِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّيَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ قَالَ أَنَا۠ أُحۡيِۦ وَأُمِيتُۖ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَأۡتِي بِٱلشَّمۡسِ مِنَ ٱلۡمَشۡرِقِ فَأۡتِ بِهَا مِنَ ٱلۡمَغۡرِبِ فَبُهِتَ ٱلَّذِي كَفَرَۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Hukumwona yule aliye hojiana na Ibrahim juu ya Mola wake Mlezi kwa sababu Mwenyezi Mungu alimpa ufalme? Ibrahim alipo sema: Mola wangu ni yule ambaye huhuisha na kufisha. Yeye akasema: Mimi pia nahuisha na kufisha. Ibrahim akasema: Mwenyezi Mungu hulichomozesha jua mashariki, basi wewe lichomozeshe magharibi. Akafedheheka yule aliye kufuru; na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu.
Humwoni yule aliye pofuka asizione dalili za Imani akajadiliana na Ibrahim, rafiki wa Mwenyezi Mungu, katika uungu wa Mola wake Mlezi na Umoja wake, na vipi alivyo danganyika na ufalme wake alio pewa na Mola wake Mlezi hata akatoka kwenye nuru ya maumbile akaingia katika kiza cha ukafiri? Alipo sema Ibrahim: Mwenyezi Mungu huhuisha na hufisha, kwa kuitia roho katika kiwiliwili na kuitoa, yule mfalme kafiri akasema: Nami nahuisha na ninafisha kwa kusamehe na kuuwa. Basi Ibrahim akamwambia ili kuyakata majadiliano: Mwenyezi Mungu analichomozesha jua mashariki, basi wewe lileta litoke magharibi kama wewe ni mungu kama unavyo dai. Akahizika, na majadiliano yakakatika kwa nguvu za hoja zilizo kashifu udhaifu wake na kughurika kwake. Na Mwenyezi Mungu hawawezeshi wakaidi na wenye inadi kufuata Haki.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (258) سۈرە: سۈرە بەقەرە
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

تاقاش