قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (75) سۈرە: سۈرە ئال ئىمران
۞ وَمِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مَنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِقِنطَارٖ يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ وَمِنۡهُم مَّنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِدِينَارٖ لَّا يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ إِلَّا مَا دُمۡتَ عَلَيۡهِ قَآئِمٗاۗ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُواْ لَيۡسَ عَلَيۡنَا فِي ٱلۡأُمِّيِّـۧنَ سَبِيلٞ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Na miongoni mwa Watu wa Kitabu yupo ambaye ukimpa amana ya mrundi wa mali atakurudishia, na miongoni mwao yupo ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii isipo kuwa ukimsimamia kumdai. Haya ni kwa kuwa wakisema: Hatuna lawama kwa ajili ya hawa wasio jua kusoma. Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu, hali nao wanajua.
Huo ndio mwendo wao Watu wa Biblia katika itikadi, ama mwendo wao katika mambo ya mali utaona: Kati yao kuna ambaye ukimpa amana ya chungu ya dhahabu au fedha atakurejeshea sawa sawa bila ya kupunguka chochote. Na mwengine kati yao ukimpa amana ya dinari moja tu hakurudushii, ila ikiwa utamshikilia mpaka aitoe. Haya ni kwa sababu wapo baadhi yao wanawaona watu wa mataifa mengine, si watu wa Biblia basi haiwalazimu wao kuwatendea haki, na wanadai kuwa hiyo ni hukumu ya Mwenyezi Mungu. Na wao wanajua vyema kuwa hayo ni kumzulia uwongo Mwenyezi Mungu. (Tazama katika Agano la Kale: Kumbukumbu la Torati, 23.19-20 inaruhusu kumnyonya riba mtu mbali asiyekuwa Yahudi. Kumbukumbu 12.21 inaruhusu kumlisha nyamafu mgeni na kumuuzia pia. Uzushi kama huu unakashifiwa na Aya 78 ifuatayo kuwa haya hayakutokana na Mwenyezi Mungu, bali wamepachika wao tu katika vitabu vyao.)
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (75) سۈرە: سۈرە ئال ئىمران
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

تاقاش