قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (5) سۈرە: سۈرە مائىدە
ٱلۡيَوۡمَ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُۖ وَطَعَامُ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حِلّٞ لَّكُمۡ وَطَعَامُكُمۡ حِلّٞ لَّهُمۡۖ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِيٓ أَخۡدَانٖۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ حَبِطَ عَمَلُهُۥ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ
Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. Na chakula cha walio pewa Kitabu ni halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. Na pia wanawake wema miongoni mwa Waumini, na wanawake wema miongoni mwa walio pewa Kitabu kabla yenu, mtakapo wapa mahari yao, mkafunga nao ndoa, bila ya kufanya uhasharati wala kuwaweka kinyumba. Na anaye kataa kuamini bila shaka a'mali yake imepotea, naye katika Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara.
Leo, yaani tangu kuteremka Aya hii, mmehalalishiwa kila kilicho chema kipendacho nafsi njema; na pia mmehalalishiwa chakula cha Watu wa Kitabu (Mayahudi na Wakristo), na walio chinja wao, katika vitu ambavyo havikutajwa kuwa ni haramu, kama ilivyo kuwa wao ni halali kwao kula chakula chenu. Na mmehalalishiwa nyinyi kuwaoa wanawake wema wa Kiislamu na wa Ahlil Kitaab (Mayahudi na Wakristo). Hayo kwa sharti mkiwapa mahari yao kwa kusudi ya kuwaoa, sio kwa kuingiana nao kinyume na sharia kwa jahara au kwa kuwaweka mahawara kinyumba. Na mwenye kuipinga Dini, basi amepoteza malipo ya a'mali yake aliyo dhani kuwa ndiyo itamkaribisha, naye huko Akhera ni katika walio hiliki.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى ئايەت: (5) سۈرە: سۈرە مائىدە
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

تاقاش