የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ * - የትርጉሞች ማዉጫ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (65) ምዕራፍ: ሱረቱ ዩሱፍ
وَلَمَّا فَتَحُواْ مَتَٰعَهُمۡ وَجَدُواْ بِضَٰعَتَهُمۡ رُدَّتۡ إِلَيۡهِمۡۖ قَالُواْ يَٰٓأَبَانَا مَا نَبۡغِيۖ هَٰذِهِۦ بِضَٰعَتُنَا رُدَّتۡ إِلَيۡنَاۖ وَنَمِيرُ أَهۡلَنَا وَنَحۡفَظُ أَخَانَا وَنَزۡدَادُ كَيۡلَ بَعِيرٖۖ ذَٰلِكَ كَيۡلٞ يَسِيرٞ
Na walipo fungua mizigo yao wakakuta bidhaa zao wamerudishiwa. Wakasema: Ewe baba yetu! Tutake nini zaidi? Hizi bidhaa zetu tumerudishiwa. Wacha tuwaletee watu wetu chakula, na tutamlinda ndugu yetu, na tutaongeza shehena ya ngamia. Na hicho ni kipimo kidogo.
Na wale nduguze Yusuf hawakujua kuwa Yusuf aliwatilia bidhaa zao katika mizigo yao. Walipo ifungua wakakuta mali yao, na wakaona hisani aliyo wafanyia Yusuf, wakaitumia hiyo kuzidi kumpoza moyo Yaa'qub, na kumkinaisha awakubalie kwa aliyo yataka Mheshimiwa. Wakazidi kumshikilia akubali, wakamkumbusha makhusiano yao yalio wafunga kwa baba mmoja. Wakasema: Ewe baba yetu! Unataka wema gani zaidi kuliko haya, na hayo yatayo kuwa? Haya mali yetu tumerudishiwa bila ya kuchukuliwa chochote. Basi natusafiri na ndugu yetu, na tuwaletee watu wetu mahitaji, nasi tutamchunga ndugu yetu, na tutaongeza mahitaji shehena ya ngamia kuwa ni haki ya ndugu yetu! Kwani yule Mheshimiwa kapanga kuwa kila mtu humpa shehena ya ngamia.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (65) ምዕራፍ: ሱረቱ ዩሱፍ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ

መዝጋት