የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ * - የትርጉሞች ማዉጫ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (93) ምዕራፍ: ሱረቱ አን-ነሕል
وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَعَلَكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَلَٰكِن يُضِلُّ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَلَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na Mwenyezi Mungu angeli taka, kwa yakini angeli kufanyeni umma mmoja. Lakini anamwachia kupotea anaye mtaka, na anamwongoa amtakaye. Na hakika mtaulizwa kwa yale mliyo kuwa mkiyafanya.
Mwenyezi Mungu ange taka angeli kufanyeni nyote umma wa namna moja kwa jinsi, na rangi, na imani, bila ya khitilafu. Na hayo ni kwa kukupeni umbo jengine, mkawa kama Malaika wasio na uwezo wa kukhiari watakalo. Lakini ametaka muwe jinsi na rangi mbali mbali, na akakupeni uwezo wa kukhiari wenyewe. Mwenye kukhiari matamanio ya dunia kuliko kumridhi Mwenyezi Mungu, anaachwa kwa ayatakayo. Na mwenye kutaka kumridhi Mwenyezi Mungu kwa vitendo vyema, anasahilishiwa kwa anayo yataka. Na kuweni na yakini kuwa nyote nyinyi mtakuja ulizwa Siku ya Kiyama juu ya mliyo yatenda duniani, na mtalipwa kwa vitendo vyenu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (93) ምዕራፍ: ሱረቱ አን-ነሕል
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ

መዝጋት