Na lau kuwa tumewaamrisha: Jiueni, au tokeni majumbani kwenu, wasingeli fanya hayo ila wachache tu miongoni mwao. Na lau kama wangeli fanya walio waidhiwa ingeli kuwa bora kwao na uthibitisho wa nguvu zaidi.
Na lau kuwa Sisi tumewalazimisha mashaka ya mwisho, kwa kuwaamrisha wapigane Jihadi moja kwa moja, na wajitolee nafsi zao kutilifu, au watoke nje waache majumba yao kwenda pigana Jihadi daima, wasinge kubali kut'ii ila wachache tu. Lakini Mwenyezi Mungu, Aliye takasika na kutukuka, hakalifishi ila linalo wezekana. Na lau kuwa wange fanya hayo na wakafuata haki yake ingeli kuwa ni kheri yao ya duniani na Akhera. Na hivyo ndiyo inavyo pelekea kuthibiti Imani, na kuingia imara, na kuleta utulivu.
Na kwa sababu ya kut'ii kwao kwa uweza wao inakuwa hakika Mwenyezi Mungu amewaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka isio pindukia kiasi kwa kuzidi au kupungua.
Na wenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume, hao wa pamoja na wale alio waneemesha Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii, na Masiddiqi, na Mashahidi, na Watu wema. Na uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!
Na mwenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume kwa kuzifuata kwa unyenyekevu amri zao na kuridhia hukumu yao, basi huyo yu pamoja na alio waneemesha Mwenyezi Mungu kwa uwongofu na kuwawezesha duniani na Akhera. Na watu hao ni Manabii wake, na wafuasi wao walio wasadiki na kuwakubali na wakafuata nyendo zao, na Mashahidi walio kufa katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na watu wema watendao mema kwa siri na dhaahiri. Na hapana la kushinda uzuri kuliko kuwa pamoja na watu hawa - haingii mashakani mwenye kukaa nao, wala hayachoshi mazungumzo yao.
Hiyo ni fadhila itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kutosha.
Hayo ni makao matukufu kwa mwenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hiyo ni fadhila kubwa inayo tokana na Mwenyezi Mungu. Naye anavijua sana vitendo vyenu, naye atakulipeni kwavyo. Yamtosha Muumini kuwa Mwenyezi Mungu anamjua, naye lake ni kumt'ii Mola wake Mlezi na kutafuta radhi zake.
Enyi mlio amini! Chukueni hadhari yenu! Na mtoke kwa vikosi au tokeni nyote pamoja!
Enyi Mlio amini! Daima kuweni na hadhari na maadui wenu. Jizatitini kupambana na vitimbi vyao. Na mkitoka kwenda vitani tokeni kwa vikosi vikosi, au tokeni nyote pamoja.
Na yupo kati yenu anaye bakia nyuma; na ukikusibuni msiba husema: Mwenyezi Mungu kanifanyia kheri sikuwa nao.
Na wahadharisheni wanao kaa nyuma wasende nanyi vitani. Miongoni mwa hao mnao ishi nao wakajizuia wasifuatane nanyi kwenda kupigana, mkipatwa na shida na masaibu katika Jihadi, wao wa kikundi hicho, kwa kufurahia yaliyo kusibuni, husema: Mwenyezi Mungu katufanyia kheri kwa kuwa hatukwenda nao vitani.
Na ikIkufikieni Fadhila kutoka kwa Mwenezi Mungu husema, kama kwamba hapakuwa mapenzi baina yenu naye, laiti ni ngekuwa baina yao nikafanikiwa Mafanikio makubwa
Na mnapo pata fadhila ya ushindi kutokana na Mwenyezi Mungu, mkapata ngawira za vita, kikundi hicho hicho, kwa kuona maya na kutamani, husema: Laiti tungeli kuwa nao katika vita hivi, nasi tukapata mafanikio ya ngawira nzuri. Na husema haya na hayo kama kwamba hapakuwepo mapenzi yoyote yaliyo wafunga wao na nyinyi.
Basi nawapigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanao uza uhai wa dunia kwa Akhera. Na anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauliwa au akashinda basi tutakuja mpa ujira mkubwa.
Ikiwa yupo kati yenu anaye bakia nyuma asende kupigana kutokana na udhaifu wa Imani yake, au ulegevu wa azma yake, basi na wapigane, kuinua Neno la Mwenyezi Mungu na kuwania Haki, wale walio uza uhai wao wa dunia kutafuta uhai wa Akhera. Na mwenye kupigana vita kwa ajili ya kunyanyua Neno la Mwenyezi Mungu na kuwania Haki, atapata moja ya mema mawili. Ama atauliwa apate fadhila ya kufa shahidi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, au atashinda, apate fadhila ya kufuzu katika dunia. Naye katika hali zote mbili atapewa na Mwenyezi Mungu ujira mkubwa katika Akhera.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
የፍለጋ ዉጤቶች:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".